Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha Kamati kuu ya Halmashauri kuu ya CCM kilichofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo. Kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM leo imemteua Sioi Sumari kuwa mgombea wa ubunge kwa tiketi ya chama hicho katika jimbo la Arumeru Mashariki , akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jioni hii katika ofisi ndogo ya CCM Rumumba Katibu mkuu wa CCM itikadi na Uenezi Nape Nnauye amesema.
"Chama hicho pia kimemteua Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa kufungua kampeni hizo na kufunga lakini pia jukumu la kampeni liko kwa wanachama wote wa CCM wakiwepo viongozi walioko eneo husika.
Chama hicho pia kimemteua Katibu wa CCM Fedha na Uchumi Bw. Lameck Nchemba Mwigulu kuwa mratibu wa kampeni hizo, Katika hatua nyingine Nape amesema "Chama kimetoa baraka kwa Tasisi ya Kupambana na rushwa TAKUKURU kuendelea na mchakato wao wa kushughulikia watu waliokamatwa na rushwa katika kura za maoni za CCM jimboni humo, na akaipongeza sana TAKUKURU kwa hatua hiyo.Uchaguzi wa Jimbo la Arumeru unafanyika tena baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Jeremiah Sumari kufariki dunia hivi karibuni.




0 comments:
Post a Comment