Mtendaji
Mkuu Taasisi isiyo ya kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt.
Naiz Majani na Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Philip Besiimire wakibadilishana
hati ya mkataba wa ushirikiano wa kusaidia matibabu ya moyo kwa watoto wanaotibiwa
katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo katika ukumbi wa JKCI iliyopo
jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi Maalum – Dar es
Salaam
Taasisi isiyo ya kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) kwa kushirikiana na Vodacom Tanzania zimesaini hati ya makubaliano maalumu ya kusaidia matibabu ya moyo kwa watoto nchini hususan wale wasiokuwa na uwezo wa kugharamia matibabu hayo wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).
Taasisi isiyo ya kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) kwa kushirikiana na Vodacom Tanzania zimesaini hati ya makubaliano maalumu ya kusaidia matibabu ya moyo kwa watoto nchini hususan wale wasiokuwa na uwezo wa kugharamia matibabu hayo wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).
Makubaliano hayo yaliyosainiwa leo jijini Dar es Salaam yanahusisha kusaidia matibabu kwa watoto wenye matatizo ya moyo na kukarabati wodi ya watoto wanaohitaji uangalizi maalum (ICU).
Akizungumza katika hafla ya kusaini makubaliano hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge aliipongeza Vodacom kushiriki katika kusaidia watoto wenye magonjwa ya moyo na kuunga jitihada zinazofanywa na Serikali kuhakikisha matibabu ya moyo yanapatikana nchini.
“Ushirikiano huu utasaidia sana kuwafikia watoto wenye magonjwa ya moyo wasiokuwa na uwezo wa kugharamia matibabu lakini pia utasaidia kukarabati wodi ya watoto wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU) hivyo kuongeza nafasi ya kutoa huduma,” alisema Dkt. Kisenge.
Dkt. Kisenge alisema takwimu zinaonesha kuwa kati ya watoto 10,000 huzaliwa nchini wakiwa na matatizo ya moyo kila mwaka, ambapo zaidi ya 4,000 huhitaji upasuaji wa haraka.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu kutoka Shirika lisilo la Kiserikali la Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naizi Majani alisema mkataba wa HTAF na Vodacom umelenga kuhakikisha kuwa watoto wanaotoka katika familia duni wanapata huduma za matibabu JKCI.
“Lengo letu ni kuwasaidia watoto wenye magonjwa ya moyo ambao wengi wao hukosa msaada ukilinganisha na watu wazima ambao hupata msaada kutoka kwa watu wengi wanaowazunguka, hivyo makubaliano yetu ni kuhakikisha tunarudisha furaha kwa watoto ambao wanapitia maumivu makali yanayotokana na maradhi ya moyo”, alisema Dkt. Naiz.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Philip Besiimire alisema Vodacom imefanya tathmini na kuona kuwa gharama za matibabu hazipaswi kuwa kikwazo cha kuokoa maisha ya watoto hivyo ikaamua kushirikian na HTAF kuokoa maisha ya watoto wanaohitaji upasuaji wa moyo.
“Tupo hapa leo kuiunga mkoni Serikali ya Tanzania kwa kusaidia watoto 150 wenye magonjwa ya moyo kupata matibabu na kurejesha matumaini kwa familia zao kwani kila mtoto anastahili nafasi ya kuishi bila kujali uwezo wa familia zao”, alisema Besiimire.
Kupitia makubaliano hayo HTAF na Vodacom wanatarajia kuongeza wigo wa upatikanaji wa huduma za upasuaji wa moyo kwa watoto nchini, hatua itakayosaidia kupunguza vifo vinavyotokana na magonjwa ya moyo kwa watoto.




0 comments:
Post a Comment