Nafasi Ya Matangazo

June 29, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uteuzi huo ni kama ifuatavyo:- 

i. Jaji Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Prof. Ibrahim Hamis Juma, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Mheshimiwa Prof. Juma anachukua nafasi ya Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax ambaye ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa; na 
ii. Dkt. Deo Mwapinga ameteuliwa kuwa Balozi. Dkt. Mwapinga ni Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wabunge wa Nchi Wanachama wa Mkutano wa Kimataifa wa Ukanda wa Maziwa Makuu (FP-ICGLR).
Posted by MROKI On Sunday, June 29, 2025 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo