Nafasi Ya Matangazo

March 28, 2025

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) akizungumza na wadau mbalimbali wa uhifadhi wa mazingira katika hafla iliyoandaliwa na Shirika la Uhifadhi wa mazingira la ‘The Nature Conservancy’ ya kuwashukuru wadau na kukuza mahusiano na washirika wa taasisi hiyo iliyofanyika usiku wa  Machi 27, 2025  jijini Arusha.
Baadhi ya washiriki wa hafla iliyoandaliwa na Shirika la Uhifadhi wa mazingira la ‘The Nature Conservancy’ ya kuwashukuru wadau na kukuza mahusiano na washirika wa taasisi hiyo iliyofanyika usiku wa  Machi 27, 2025  jijini Arusha wakimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb)(hayupo pichani) alipokuwa  akizungumza nao.
Mkurugenzi Mkuu wa  Kanda ya Afrika wa Shirika la  Nature Conservancy, Ademola Adjagbe akizungumza kuhusu umuhimu wa kushirikiana katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kukuza uhifadhi, katika hafla iliyoandaliwa na Shirika la Uhifadhi wa mazingira la ‘The Nature Conservancy’ iliyofanyika usiku wa Machi 27,2025 jijini Arusha.
Baadhi ya washiriki wa hafla iliyoandaliwa na Shirika la Uhifadhi wa mazingira la ‘The Nature Conservancy’ ya kuwashukuru wadau na kukuza mahusiano na washirika wa taasisi hiyo iliyofanyika usiku wa  Machi 27, 2025  jijini Arusha wakimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb)(hayupo pichani) alipokuwa  akizungumza nao.
************
Na Happiness Shayo-Arusha
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) amesema kuwa jamii zimeendelea kunufaika na biashara ya hewa ukaa kupitia miradi ya  Shirika la Uhifadhi wa mazingira la ‘The Nature Conservancy’ nchini Tanzania lililojikita katika kuhifadhi mifumo ya ikolojia , kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi pamoja na kuongeza mapato kwa jamii.
 
Ameyasema hayo katika hafla ya kuwashukuru wadau na kukuza mahusiano na washirika wa taasisi hiyo iliyofanyika usiku wa  Machi 27, 2025  jijini Arusha.
 
“Tunashukuru sana kwa msaada wa The Nature Conservancy, hasa kwa kushirikiana na Carbon Tanzania, kuanzisha miradi ya kaboni katika maeneo muhimu kama vile Yaeda Chini, Makame Wildlife Management Area (WMA), Ntakata, na misitu ya Tongwe. Ushirikiano huu sio tu unasaidia kulinda mifumo muhimu ya ikolojia lakini pia hutoa fursa muhimu kwa jamii za wenyeji kufaidika kupitia mbinu bunifu za uhifadhi na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi” amesema Mhe.Chana.

mefafanua kuwa kupitia biashara ya kaboni Msitu wa Ntakata ulio chini ya Serikali ya vijiji, wilaya ya Tanganyika, umeingiza dola milioni 24 katika mapato kwa jamii tangu Juni 2019 na kwamba Carbon Tanzania inaendelea kuhakikisha jamii katika vijiji 8 inapata dola milioni 12 kila mwaka (takribani tzs bilioni 3 hadi 4 kila mwaka).
 
Mhe. Chana ameitaka taasisi hiyo kuendelea kuhakikisha inafanya kazi karibu zaidi na jamii ili zifaidike na miradi hiyo.
 
Aidha, amesisitiza taasisi hiyo kushirikiana na Serikali hasa katika kujenga na kuandaa maabara ya kisasa katika Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Afrika-MWEKA.
 
“Kituo hiki kitaboresha sayansi ya uhifadhi, kutoa mafunzo kwa vitendo katika maeneo kama vile kutambua kwa mbali, baiolojia ya molekuli, sayansi ya mimea/herbariamu, na kemia ya mazingira. Kwa kuandaa kizazi kijacho cha viongozi wa uhifadhi na zana hizi za hali ya juu, tunalenga kuunga mkono utafiti unaotumika ambao unaweza kufuatilia mikopo ya bioanuwai, kuchanganua viwango vya uchafuzi wa mazingira katika mazingira yetu ya mijini na kando ya miji, na kuchangia juhudi za uhifadhi wa bahari na utafiti wa jamii” amesema Mhe. Chana.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa  Kanda ya Afrika wa Shirika la  Nature Conservancy, Ademola Adjagbe  amesema kuwa Shirika hilo linafanya kazi katika nchi zaidi ya 80 duniani katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za uhifadhi wa mazingira.

Ameongeza kuwa Afrika inakabiliwa na changamoto mbalimbali za kimazingira zinazopelekea upotevu wa rasilimali hivyo ni vyema kushirikiana kuhakikisha  Maliasili zinaokolewa, maisha ya binadamu yanalindwa, kukabiliana na  changamoto za mabadiliko ya tabianchi na kutunza baioanuwai.

Hafla hiyo imehudhuriwa na  Viongozi mbalimbali kutoka Shirika la The Nature Conservancy’s, wadau mbalimbali wa uhifadhi kutoka Serikalini na Sekta Binafsi.
Posted by MROKI On Friday, March 28, 2025 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo