December 30, 2022
Amesema ni vema balozi hizo zikaanzisha majukwaa ya kiuchumi yatakayowakutanisha wafanyabiashara na wawekezaji wa nchi hizo katika sekta mbalimbali za kiuchumi ikiwemo ardhi, madini, utalii, mawasiliano na biashara.
“Muwasihi wafanyabiashara na wawekezaji waje kuwekeza Tanzania na washirikiane na Watanzania kufungua makampuni, hii itatusaidia Watanzania kubadilishana uzoefu wa namna bora ya kuendesha biashara.”
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Desemba 30, 2022) wakati akizungumza na watumishi wa ubalozi wa Tanzania ulioko jijini Pretoria, Afrika Kusini.
Amesema watumishi wa balozi za Tanzania hawana budi kuandaa makubaliano baina ya Tanzania na nchi walizoko ambayo yataonesha nini kinatakiwa nchini humo na ambacho kinapatikana kwa wingi nyumbani Tanzania.
“Hapa kwenu, ubalozi unapaswa kutengeneza makubaliano maalum ya kibiashara miongoni mwa nchi hizi mbili na kubainisha aina ya bidhaa ambazo zinapatikana Tanzania kwa wingi na zinahitajika Afrika Kusini,” amesisitiza.
Aidha, Waziri Mkuu amesema ni vema pia ubalozi huo ukaendelea kuhamasisha watalii kutoka nchini humo kwa kubainisha vivituo vya utalii vilivyoko Tanzania ambavyo nchi hiyo haina huku akitolea mfano Mlima Kilimanjaro.
Awali, akitoa taarifa ya kiutendaji ya ubalozi huo, Kaimu Balozi Peter Shija alisema Tanzania inaweza kunufaika zaidi na fursa za biashara zilizopo nchini humo kwa kuuza mazao kama, mchele, maharage, korosho na mazao ya matunda.
Na Englibert Kayombo, WAF - Dar Es Salaam.
December 29, 2022
Mbunge wa Makete Mhe. Festo Sanga akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Makete kabla ya hafla ya utiaji saini Mkataba wa ujenzi wa barabara ya Kitulo hadi Iniho KM 36.3 kwa kiwango cha Lami, iliyofanyika Wilayani Makete, Mkoani Njombe.
Akizungumza katika hafla ya utiaji saini ujenzi wa barabara ya Isyonje-Kikondo hadi Makete KM 96.2 sehemu ya Kitulo hadi Iniho KM 36.3 inayojengwa kwa kiwango cha lami Waziri Prof. Mbarawa amesema Serikali ya awamu ya sita itahakikisha inaunganisha kwa njia fupi mikoa ya Mtwara, Ruvuma, Njombe hadi Mbeya kupitia Makete ili kukuza fursa za kiuchumi zilizoko katika ushoroba huo.
“Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia imejikita kwenye kuboresha miundombinu hususani maeneo yenye uzalishaji mkubwa hivyo niwahakikishie kuwa ongezeni uzalishaji miundombinu bora inakuja,’ amesisitiza Waziri Prof. Mbarawa.
Ameitaka Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), kumsimamia kikamilifu Mkandarasi anayejenga barabara hiyo M/S China National Aero-Technology Egineering Corporation ili mradi huo ukamilike kwa wakati na viwango.
Mtendaji mkuu wa TANROADS Mhandisi Rogatus Mativila amesema ujenzi wa barabara hiyo utahusisha ujenzi wa mizani katika Kijiji cha Igalala ili kudhibiti magari yanayozidisha uzito hivyo kuwataka wananchi kuzingatia sheria na kulinda miundombinu yote ya barabara.
Kwa upande wake Mbunge wa Makete Festo Sanga ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha kwa ajili ya mradi huo kwani kukamilika kwake kutaunganisha wilaya hiyo na Mkoa wa Mbeya kwa njia fupi, kukuza utalii wa hifadhi ya taifa Kitulo na kupandisha thamani ya mazao mbalimbali yanayozalishwa Mkoani Njombe.
Mkuu wa mkoa wa Njombe Bw, Anthon Mtaka amewataka wakazi wa wilaya ya Makete kote nchini kutumia maendeleo ya ujenzi wa miundombinu kuwekeza wilayani humo.
Zaidi ya shilingi bilioni 69.7 zinatarajiwa kutumika katika ujenzi huo unaotarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha miezi 36.
Wahitimu wa Shahada ya Utabibu yaani “ Doctor of Medicine” Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) wakila kiapo cha Utii na Uadilifu wa kazi yao, baada ya kutunukiwa Shahada ya Utabibu na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambae pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, katika Mahafali ya 18 ya Chuo hicho yaliyofanyika katika Ukumbi wa Dk.Ali Mohamed Shein Tunguu Wilaya ya Kati Unguja leo 28-12-2022.
Wahitimu wa Cheti cha Uongozi wa Fedha yaani ”Certificate in Financial Administration” wakishangia baada ya kutunukiwa Cheti katika Mahafali ya 18 ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambae pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Dk.Ali Mohamed Shein Tunguu Wilaya ya Kati Unguja leo 28-112-2022.
December 28, 2022
Akizungumza na wanafamilia kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Samia, Waziri Mkuu amewasilisha salaam za pole kutoka kwa Mheshimiwa Rais na kusema Mheshimiwa Rais anafuatilia hali ya Mheshimiwa Lowassa kwa ukaribu na anamuombea afya njema.
Waziri Mkuu ametoa salamu hizo leo (Jumatano, Desemba 28, 2022) jijini Johannesburg, Afrika Kusini ambako alienda kumjulia hali Mheshimiwa Lowassa.
Kwa upande wake, Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu, Mama Regina Lowassa amemshukuru Mheshimiwa Rais kwa jinsi ambavyo amekuwa karibu na wanafamilia na namna ambavyo anafuatilia matibabu ya mpendwa wao.
Naye mtoto mkubwa wa Mheshimiwa Lowassa na Mbunge wa Monduli, Bw. Fredrick Lowassa amewashukuru Watanzania kwa maombi yao ya kumtakia afya njema baba yao.
Walengwa wa Tasaf wilayani sikonge mkoani Tabora wameshauriwa kulima mazao yanayo stahimili ukame kulingana na kuwepo kwa mvua kidogo inayoratajia kunyesha msimu huu wa kilimo.
Wito huo umetolewa jana na Afisa Kilimo kata ya Pangale na Mwezeshaji wa walengwa wa Tasaf Josephine Mzoo wakati wa uhawilishaji uliofanyika katika kijiji cha kipanga kata ya kipanga Mlimani wilayani Sikonge mkoani hapo.
Alisema kwamba wakulima wanapaswa kulima mazao kinga njaa ambayo ni Viazi na Mihogo ili kuweza kukabilia na njaa inayoweza kujitokeza katika msimu wa kilimo mwaka huu .
Josephine aliendelea kusema kwamba mvua za mwaka huu ni chache kulingana na utabiria wa hali ya hewa unaonyesha kuwa mvua zitanyesha chini ya wastani.
Naye mlengwa wa Tasaf katika kjiji cha Kipanga mlimani na kata ya Kipanga Nelea Katumbo alisema kwamba watajitaidi kulima mazao yanayostamili ukame ili kuweza kupata chakula katika msimu huu wa kilimo .
Alisema kwamba licha ya kulima mazao hayo pia amefanikiwa kufunga kuku na kisha kuweza kununua mbuzi na sasa ana mbuzi 11 ambao analengo la kuunza a kununua Ng’ombe.
Naye Zafarani Hussein alisema kwamba kulingana utabiri wa hali ya hewa unaosema mvua za mwaka huu zitanyesha chini ya wastani jambo ambalo wanalazimika kulima mazao yanayostahimili ukame.
Alisema ushauri huo ulitolewa na afisa kilimo wanauchukuwa kwa jicho la Tatu kutokana na mvua kunyesha kwa kiwango kidogo ila watajitaidi kuyatunza mazao ambayo tayari wameyapanda .
Hata hivyo malengo hayo amekiri kunufaika na mpango wa kunusuru kaya masikini – Tasaf kwa kuweza kusomesha watoto, kuanzisha miradi kufunga mbuzi ,kuku, bata na Ngombe.
Alisema kuwa tangu ajiunge na TASAF ambapo kwa mwaka huu ameweza kulima na anatarajia kupata gunia 8 za mahindi, lengo ni kuongeza kulima mazao ya kilimo hasa Karanga, Muhogo na kuongeze idadi ya kutoka mbuzi 10 hadi kununua Ng’ombe wa 3 kwa ajili ya kumsaidia kulima mashamba yake .
Alisema kwamba licha ya kununua Ng’ombe hao pia amenunua jembe la kukokotwa na Ng’ombe kitu ambacho kitamsaidia kulima mashamba makubwa kikubwa kuona mvua inayesha vizuri .
“Tunaishukuru sana serikali kwa kutuondolea umaskini huku vijijini kwetu, kama sio fedha hizo mimi ningekuwa nimeshakufa, lakini kutokana na fedha hizo zimemsaida kimaendeleo”alisema Zafarani Husein
Mratibu wa mfuko wa maendeleo ya Jamii wilaya ya sikonge’ Claud Nkanwa Alisema walengwa wameendelea kupewa mafunzo ya kujiwekeza katika raslimali zalishi ili pindi mpango huo utakapoisha au kipindi chao kitakapoisha waweze kujiwezesha kuendelea na Maisha yaliyo bora .
Hata hivyo aliwataka wananchi wanaonufaika na mpango huo wa kunusuru kaya masikini TASAF kuzitumia fedha hizo kama ambavyo wamekuwa wakifundishwa na viongozi wa TASAF huku akisema yeye atakuwa mfuatiliaji wa fedha hizo.
Zaidi ya shilingi bilioni 38 fedha za ndani zinatarajiwa kutumika katika ujenzi huo ambao pia utahusisha taa za barabarani.
December 27, 2022
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Abel Philip amekabidhi gari aina ya Toyota Coaster lenye namba ya usajili STM 2639 kwa MkurugenzI Msaidizi wa Utawala na Rasimali Watu, Zahara Guga Desemba 27, 2022 Jijini Dodoma kwa shughuli kadhaa za utendaji.