Nafasi Ya Matangazo

June 27, 2022

CHAMA cha Wasafirishaji Tanzania (TAT) kinampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan na Serikali kwa ujumla kwa kusikiliza na kufanyia kazi maoni ya Wasafirishaji nchini kwenye Bajeti ya Mwaka 2022/2023.

Taarifa kutoka Ofisi ya Rais wa TAT, Mohammed Abdullah, ya mwishoni mwa wiki, imesema: “Kwa niaba ya Chama cha Wasafirishaji Tanzania (TAT), Bodi, Wanachama na Wasafirishaji wote nchini, tunapenda  kukupongeza  Mh.Samia  Suluhu  Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na wasaidizi wako kwa kuwasikiliza Wasafirishaji wa mizigo katika Bajeti ya Mwaka 2022/23.

 Tunayo furaha kubwa kukupa pongezi za dhati kabisa pamoja na wataalamu wako ambao wamekuwa wakifanya kazi nzuri kuishirikisha Sekta Binafsi katika masuala mbalimbali ya Bajeti na Kodi.

 “Tunashukuru sana kwa punguzo katika Kodi ya Matrela na Vichwa vya Magari ya kusafirishia mizigo hadi 0%, na Punguzo katika Tozo ya matumizi ya barabara kutoka dola za Marekani 16 kwa kilomita 100 hadi dola 10 kwa kilomita 100.

 Tunakupongeza Rais Mama Samia Suluhu Hassan na Serikali yako kwa kuwa sikivu kwa maombi ya Wasafirishaji nchini na tuna imani kubwa kuwa changamoto ambazo hazijatatuliwa, zitafanyiwa marekebisho ili zilete tija katika Sekta ya Usafirishaji  na  nchi  kwa ujumla.”

 TAT ni chama chenye wanachama wasafirishaji wa mizigo na mafuta zaidi ya 200 nchini. Changamoto katika Sekta ya Usafirishaji zinawagusa moja kwa wanachama wake na Wasafirishaji wote nchini.
Posted by MROKI On Monday, June 27, 2022 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo