Nafasi Ya Matangazo

October 10, 2019

CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

TAARIFA KWA UMMA

KUHUSU MCHAKATO WA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA NA VIJIJI MWAKA 2019
_______________

Ofisi ya Makao Makuu, Dodoma
10 Oktoba 2019

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinapenda kuujulisha umma wa wanachama wa CCM kuwa Mchakato wa kuwapata wana CCM watakao simama katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Vijiji unaendelea ndani ya Chama.

Ufuatao ni mtiririko wa matukio ndani ya Chama ambao wanachama, viongozi na wanaoomba kufikiriwa na kuteliwa na Chama wanapaswa kuuzingatia;-

NGAZI YA VIJIJI NA MITAA

Tarehe 7 – 12 Oktoba, 2019: Kuchukua na kurejesha fomu za kuomba kugombea Uenyekiti wa Mitaa, Vijiji na Ujumbe wa Serikali za Vijiji na Mitaa kwa Makatibu wa Matawi ya CCM kote nchini.

Tarehe 13 Oktoba, 2019: Kamati za Siasa za Matawi kujadili wagombea na kutoa Mapendekezo yake kwa Kamati za Siasa za Kata

Tarehe 14 – 15 Oktoba, 2019: Kamati za Siasa za Kata kujadili wagombea na kutoa mapendekezo yake kwa Kamati za Siasa za Wilaya

Tarehe 16 – 18 Oktoba, 2019: Kamati za Siasa za Wilaya kujadili wagombea na kufanya uteuzi wa wagombea kwa ajili ya kupigiwa kura za maoni na Mkutano wa Wanachama wote wa Tawi.

Tarehe 19 – 20 Oktoba, 2019: Mikutano ya kura za Maoni ya nafasi ya Mwenyekiti wa Mtaa au Kijiji – Mkutano wa Wanachama wote wa Tawi

BAADA YA KURA ZA MAONI

Tarehe 21 Oktoba, 2019: Kamati za Siasa za Halmashauri Kuu za Matawi kujadili wagombea na kutoa mapendekezo yake kwa Kamati za Siasa za Halmashauri Kuu ya Kata

Tarehe 22 – 23 Oktoba, 2019: Kamati za Siasa za Halmashauri Kuu za Kata kujadili wagombea na kutoa mapendekezo yake kwa Kamati za Siasa za Wilaya

Tarehe 24 – 26 Oktoba, 2019: Kamati za Siasa za Halmashauri Kuu za Wilaya kujadili wagombea na kutuma mapendekezo yake kwa Halmashauri Kuu ya CCM ya Wilaya.

Tarehe 27 – 28 Oktoba, 2019: Halmashauri Kuu ya CCM ya Wilaya Kufanya Uteuzi wa Mwisho wa Wanachama watakaogombea Uenyekiti wa Mtaa, Ujumbe wa Kamati ya Mtaa, Uenyekiti wa Kijiji na Ujumbe wa Halmashauri ya Kijiji.

NYONGEZA: RATIBA YA SERIKALI

Tarehe 8 – 14 Oktoba, 2019: Zoezi la uandikishaji wapiga kura siku saba tu kwa Mwananchi mkaazi wa Mtaa/ Kijiji na Kitongoji

Tarehe 29 Oktoba, 2019: Kuanza kuchukua fomu za kugombea

Tarehe 4 Novemba, 2019: Tarehe ya Mwisho ya kurejesha fomu kwa Msimamizi

Tarehe 10 Novemba, 2019: Uwasilishaji wa ratiba za kampeni kwa Msimamizi

Tarehe 17 – 23 Novemba, 2019: Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji

Tarehe 24 Novemba, 2019: Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji

Uongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) chini ya Ndugu John Pombe Joseph Magufuli, Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unasisitiza wale wote wenye sifa na wamekidhi vigezo na masharti ya uanachama wajitokeze kuchukua fomu na kuomba kufikiriwa na hatimaye kuteuliwa. Fomu zinatolewa bure katika Matawi ya CCM.

Tunatoa rai kwamba Chama kinatarajia wana CCM wenye kuishi misingi ya Chama chetu watu mahodari wa uadilifu, uaminifu, unyenyekevu, Wachapa kazi, wenye kazi zinazowaletea kipato halali, watetezi wa kweli wa Maslahi ya wananchi, wanaochukizwa na rushwa na ubadhirifu wa mali za umma wajitokeze ili wakakamilishe safu ya uongozi wa Serikali ya CCM inayotoa uongozi na kuleta maendeleo makubwa kwa haraka katika nchi yetu chini ya Ndg. John Pombe Joseph Magufuli.

Wanawake na vijana wanahamasishwa kujitokeza kwa wingi kugombea.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Imetolewa na,




HUMPHREY POLEPOLE
KATIBU WA NEC – ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI   

Posted by MROKI On Thursday, October 10, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo