Nafasi Ya Matangazo

July 01, 2019

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt, Faraji Kasidi Mnyepe amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi wa benki mbalimbali, wawakilishi wa kampuni za utalii, viongozi wa vyama vya wamiliki wa vyombo vya usafiri na wafanyabiashara mbalimbali jijini Dar Es Salaam. Katika Mkutano huo, Dkt. Mnyepe aliwasihi wawakilishi hao kujipanga vizuri ili waweze kuchangamkia fursa za Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika nchini Mwezi Agosti 2019. Aliwasihi kujipanga vizuri katika maeneo mbalimbali yakiwemo ya usafiri, utalii, burdani na vyakula. Dkt. Mnyepe alisisitiza umuhimu wa Watanzania kuendeleza utamaduni wa ukarimu na kuwa waaminifu na uadilifu katika kuhudumia ugeni huo mkubwa ambapo inakadiriwa zaidi ya watu elf moja watakuja nchini.
Sehemu ya washiriki wa mkutano huo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya maandalizi ya Habari, Machapisho na Matangazo ambaye pia ni Mkurugenzi Msaidizi Kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi. Zamaradi Kawawa. 
Ujumbe ulioshiriki kikao hicho ukisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Katibu Mkuu.
Mkutano ukiendelea.
Posted by MROKI On Monday, July 01, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo