Nafasi Ya Matangazo

January 20, 2019

 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange pamoja na wajumbe wa bodi wakipewa maelezo juu ya mfumo wa usambazaji wa maji kutoka katika tanki la Makongo jijini Dar es Salaam. Bodi hiyo inafanya ziara ya siku tatu ili kuweza kujifunza na kujionea jinsi mifumo ya usambazaji wa maji kwa jiji la Dar es Salaam na Pwani. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
 Mashine zilizofungwa katika tanki la makongo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange pamoja na wajumbe wa bodi wakionyeshwa mtambo wa kuendeshea maji. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Wakiangalia mfumo wa Tenki la SalaSala jijini Dar es Salaam ikiwa ni ziara yao ya kujifunza masual mbali mbali ya maji.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange pamoja na wajumbe wa bodi  wakiwa wamewasili kituo cha mtambo wa Ruvu chini- eneo la Bagamoyo - Pwani. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange pamoja na wajumbe wa bodi wakiongea na wafanyakazi wa DAWASA kituo cha mtambo wa Ruvu chini- eneo la Bagamoyo - Pwani. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange pamoja na wajumbe wa bodi wakiongea wakiangalia zoezi la kutandika mabomba ili kuwagawia maji wakazi wa Goba -Kizudi jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa uzalishaji na usambazaji maji wa DAWASA, Injinia Aron Joseph akiwaonyesha Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA iliyoongozwa na Mwenyekiti wao Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange jinsi maji yanavyovunwa katika Mtambo wa Ruvu Chini - eneo la Bagamoyo - Pwani.
Wakikagua eneo la mto Ruvu chini...
Mkurugenzi wa uzalishaji na usambazaji maji wa DAWASA, Injinia Aron Joseph akiwaonyesha Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA iliyoongozwa na Mwenyekiti wao Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (kwanza kulia) pampu za kuvuta maji.
Meneja wa DAWASA ofisi ya Bagamoyo, Alexander Ng'wandu akitoa maelezo machache mbele ya Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA iliyoongozwa na Mwenyekiti wao Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange mara baada ya kutembelea ofisi hizo zilizopo mjini Bagamoyo - Pwani.
Meneja wa DAWASA ofisi ya Bagamoyo, Alexander Ng'wandu akitoa maelezo machache mbele ya Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA iliyoongozwa na Mwenyekiti wao Jenerali Mstaafu Davis mara baada ya kutembelea tenki  la maji la Bagamoyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange pamoja na wajumbe wa bodi wakiongea na wanahabari mara baada ya kumaliza kutembelea kituo cha mtambo wa Ruvu chini- eneo la Bagamoyo - Pwani.
Posted by MROKI On Sunday, January 20, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo