Nafasi Ya Matangazo

July 11, 2017

Kamati ya Olympic Duniani imeipa tena SuperSport kibali cha kurusha matangazo ya michuano ya Olympic kuanzia mwaka 2018 hadi 2024 barani Africa Kusini mwa jangwa la Sahara.

Makubaliano hayo kati ya kamati hiyo (International Olympic Committee IOC) yanamaanisha kuwa Supersport imepata haki ya kurusha michuano hiyo katika eneo hili la Africa. Michuano hiyo ni pamoja na ile ya  PyeongChang 2018, Tokyo 2020, Beijing 2022 na ile ya mwaka 2024 ambayo bado haijaamuliwa itafanyika katika nchi gani.

Tangazo hilo limetolewa baada ya kukamilika kwa mchakato wa kutoa zabuni kwa warusha matangazo katika kanda hii ya Afrika  - Kusini mwa Sahara. Kwa minajili hii, SuperSport pia itashirikiana na IOC katika kusaidia na kuongeza ufahamu na umaarufu wa michuano hiyo barani Africa.

Rais wa IOC Thomas Bach amekarikiwa akisema: “Tunafurahi sana kufanya kazi tena na DStv SuperSport hususan katika kuwahakikishia wapenzi wa michuano hii fursa ya kuishuhudia popote walipo katika kanda hii ya Afrika – Kusini mwa Sahara. 

Binafsi nimetembelea nchi mbalimbali barani Afrika na nimeshuhudia ushabiki mkubwa uliopo kwa michuano hii. IOC hutumia asilimia 90 ya mapato yake ya tokanayo na mikataba ya kibiashara katika kuendeleza michezo kote duniani ikiwemo Afrika”.

Naye Gideon Khobane, Afisa Mkuu wa SuperSport amesema  “Sisi tukiwa kama wadau wa muda mrefu na washirika  wa IOC, tumefurahi sana kuingia makubaliano haya na mdau wetu. Michuano hii inawatazamaji wengi sana  kutokana na umaarufu wake na umahiri mkubwa wa kimichezo unaoonyeshwa na hivyo kuwa kivutio kikubwa sana kwa watazamaji. 

Tunaimani kwa kupitia DStv SuperSport, tunawapa haki mamilioni wa washabiki wa michezo barani Afrika fursa ya kushuhudia michezo ya Olympic, moja ya mashindano makubwa kabisa duniani na yenye msisimko mkubwa”.

SuperSport ni manguli wa kurusha matangazo ya michezo barani Afrika. SuperSport ina chaneli 37 zinazorusha matangazo ya michezo mbalimbali kuanzia  michezo mikubwa kama vile kandanda pamoja na michezo midogomidogo na ile inayochipukia. Supersport huonekana katika nchi 54 Afrika – kusini mwa sahara pamoja na visiwa vya jirani.
Posted by MROKI On Tuesday, July 11, 2017 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo