Nafasi Ya Matangazo

December 13, 2015

 Waziri Mkuu Mh.Kassim Majaliwa (kulia) akimkabidhi  kombe la tuzo ya mwajiri bora kwa Mkurugenzi wa Raslimali Watu wa TBL Group,David Magese (Kushoto) katika hafla iliyoandaliwa na Chama Cha Waajiri Tanzania na kufanyika katika ukumbi wa Mlimani City mwishoni mwa wiki ambapo TBL iliibuka kwa mshindi wa tuzo hiyo kwa mwaka 2015,(katikati) ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck sadiki.
 Mkurugenzi wa Raslimali Watu wa TBL Group,David Magese  akionyesha kombe la tuzo ya mwajiri bora ambalo kampuni yake imeibuka kuwa mshindi mwaka huu katika hafla iliyoandaliwa na Chama Cha Waajiri Tanzania na kufanyika katika ukumbi wa Mlimani City mwishoni mwa wiki.
 Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya TBL group wakiwa katika picha ya  pamoja muda mfupi baada ya kampuni yao kuibuka mshindi wa jumla wa tuzo ya mwajiri bora inayotolewa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City mwishoni mwa wiki.


Waziri Mkuu Mh.Kassim Majaliwa ( wa nne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa serikali,viongozi wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) na wafanyakazi wa kampuni ya TBL Group muda mfupi baada ya kuitunukia kampuni hiyo tuzo ya mwajiri bora kwa mwaka huu katika hafla iliyoandaliwa na Chama Cha Waajiri Tanzania na kufanyika katika ukumbi wa Mlimani City mwishoni mwa wiki. SOMA ZAIDI BOFYA HAPA



 ***********
 KAMPUNI ya Tanzania Breweries Limited  Group  imeibuka mshindi wa tuzo bora kwa mwaka 2015.Tuzo za mwajiri bora wa mwaka hutolewa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) nchini kwa kampuni inayokidhi vigezo mbalimbali vya mazingira mazuri ya kufanyia kazi nchini.

Mgeni wa heshima katika hafla ya Chama Cha Waajiri nchini kutunuku tuzo hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa  Mlimani City alikuwa ni Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa.TBL ambayo  pia inashikilia tuzo ya Mlipa Kodi bora nchini pia katika shindano hili lililoshirikisha makampuni mengi nchini ilishinda tuzo zingine tofauti ambazo ni Uzingatiaji

Kanuni Bora za Uongozi,Uongozi na Utawala,Uzingatiaji wa Kanuni za Raslimali Watu ,Ubora na Uzalishaji,Kujali na kuthamini walemavu na tuzo ya Taasisi Bora inayoongoza kwa Ukubwa .

Mwaka jana kampuni ya TBL ilishinda tuzo ya jumla katika kipengele cha Mahusiano mazuri na wafanyakazi ambayo inadhihirisha kuwa kampuni imeweka mazingira bora ya kufanyia kazi na inawajali wafanyakazi wake katika ngazi zote.Tuzo hiyo pia ilitambua kuwa TBL imejenga mazingira bora na uongozi makini unaozingatia vigezo bora vya ajira na kujenga mazingira mazuri ya kazi kwa waajiriwa wake.

Akiongea wakati wa hafla hiyo,Mkurugenzi wa Raslimali Watu wa TBL Group David Magese alisema kuwa kampuni hiyo inao wafanyakazi 2,100 nchini kote wakiwa wanafanya kazi za ufundi,Mauzo na Usambazaji,na katika vitengo mbalimbali vya biashara na kati ya hao wapo wenye ajira za kudumu na ajira za muda.

Magese pia alisema kuwa kampuni katika kuwajali wafanyakazi wake inao utaratibu wa kuwapatia
MOTISHA ambazo zimekuwa zikitolewa kwa kuzingatia  kigezo cha utendaji wao bora wa kazi kwenye maeneo yao wanayofanyia kazi na utaratibu huu umekuwa ukiwajengea wafanyakazi kufanya kazi kwa ufanisi na kuleta tija kwa kampuni kutokana na kuwajali na kuthamini mchango wao katika maendeleo ya biashara za kampuni.

Aliendelea kueleza kuwa TBL inao mpango maalumu wa kutoa elimu ya tahadhari kwa wafanyakazi wake dhidi ya magonjwa mbalimbali ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza kwa ajili ya kulinda afya za afanyakazi na  chini ya mpango huu imejipangia utaratibu wa kutoa  elimu ya afya kuendana na siku za matukio mbalimbali yanayohusiana na afya na usimamizi wake unafanyika kwa umakuni mkubwa chini ya wasimamizi wenye ujuzi unaostahili.

Magese pia alisema kampuni imekuwa na utaratibu wa kutoa mafunzo mbalimbali kwa wafanyakazi wake ambayo yanawawezesha kufanya zao kwa ufanisi na  bila kusimamiwa.”Bajeti ya asilimia 50% ya kitengo cha Rasilimali watu imekuwa ikitumika kwa ajili ya kutoa mafunzo ya kuwapatia ujuzi afanyakazi kwa kuwa kampuni inaamini kuwa wafanyakazi bora na wenye ujuzi ndio nguzo katika uzalishaji na kukuza biashara zake”.Alisema.
Posted by MROKI On Sunday, December 13, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo