Nafasi Ya Matangazo

September 22, 2015

Na Woinde Shizza,Arusha
Baada ya kutokuwepo kwa mbio za riadha zijulikanazo kama mount meru Marathon kwa miaka 15 sasa ,hatimaye wadau wa mchezo wamjitokeza na kurudisha mbio hizo ambazo zinatarajiwa kufanyika  octoba 4 jijini Arusha.
Mbio hizo za km 21 zilifanyika mara ya mwisho mwaka 2000,ambapo hazikuendelea tena kutokana na kukosa wadhamini hali iliyopelekea kukosa hamasa kwa wanariadha  mabalimbali.
Katibu wa chama cha riadha mkoani hapa  Alfredo Shahanga alisema kwuwa mbio hizo ni za wazi na zitashirikisha wanariadha wanawake na wanaume mbalimbali  kutoka ndani na nje ya nchi  kwa wanariadha ambao watakuwa  tayari kuja kushiriki.

“Mashindano haya chimbuko lake ni mkoani hapa na mara ya mwisho kufanyika ilikuwa ni mwaka 2000 kipindi hicho yakiitwa ‘Mount meru International Marathon’ yalishindwa kuendelea kufanyika kutokana na  kuwa wale waandaaji wa miaka hiyo walifikia mahali  mahali wakasitisha kutokana na sababu za kifedha”alieleza Shahanga.

Mbio hizo zinaandaliwa na Mambo jambo digital centre kwa kushirikiana na chama cha riadha mkoani hapa  zitaanzia mnara wa saa  zitazunguka kuelekea barabra ya sokoine mpaka uwanja wa ndege baadae zitamalizikia uwanja wa mpira wa sheikh Amri Abeid.
Shahanga  ambaye pia ni katibu wa Chama cha Riadha
Posted by MROKI On Tuesday, September 22, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo