Nafasi Ya Matangazo

July 14, 2015


USIKU wa kumkia jana Jeshi la Polisi lilipata pigo kubwa kufuatia vifo vya askari wake 4 na mwingine kujeruhiwa baada ya watu wenye silaha kuvamia kitio Kikuu cha Polisi Stakishari Ukonga.

Kituo hiki ni kikubwa kwani ni Kituo Kikuu cha Wilaya ya Kipolisi ya Ukonga, katika Kanda maalum ya Dar es Salaam ambacho kina wajibika katika mkoa wa Kipolisi Ilala.

Naandika hapa huku nikiwa na majonzi na huzuni kubwa kufuatia vifo vya wapendwa wetu hawa. Pia walikufa raia watatu huku mmoja akihisiwa kushiriki katika tukio hilo na kuuwawa na wenzake hao.

Hili la Ukonga Stakishari limetokea wakati bado hatujasahau yaliyotokea katika vituo vingi vya Polisi kama Newala, Ikwiriri, Kimanzichana na Bukombe ambapo iliripotiwa jumla ya silaha 41 zimeporwa na baade 32 kupatikana lakini pia askari zaidi ya 5 kuuwawa. 

Tukio hili la Ukonga Stakishari limetokea ikiwa imepita miezi minne tangu Rais jakaya Kikwete alipozungumzia wimbo hilo la mashambulizi kwenye vituo vya polisi nchini.

Rais Kikwete akihutubia taifa miezi minne iliyopita, alisema kuwa  polisi wanachunguza sababu ya uvamizi huo. Bila shaka na ninaamini kuwa uchunguzi huo ulisha baini sababu ya uvamizi huo.

Lakini jana tumeshuhudia tena jinamizi hilo la uvamizi na uwaji wa Polisi vituoni nchini ukianza tena baada ya kimya cha muda mrefu na wananchi tuliamini kudhibitiwa kwa hali hiyo. Soma Zaidi Hapa
Posted by MROKI On Tuesday, July 14, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo