Nafasi Ya Matangazo

July 15, 2015



Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya Huawei Technologies Tanzania, Samson Majwala (kushoto) akiwa na Meneja Mkaazi wa Huawei nchini, Zhang Junliang wakionesha simu mpya aina ya Huawei P8 wakati wa uzinduzi wake katika soko la Tanzania jijini Dar es Salaam leo.
IMG_7894 Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya Huawei Technologies Tanzania, Samson Majwala akiielezea simu muundo wa simu hiyo Huawei P8.
IMG_7856
Meneja Mkazi anayeshughulikia bidhaa za kampuni ya Huawei Tanzania, Bw. Zhang Junliang, akitoa taarifa fupi ya simu ya Huawei P8 mbele ya waandishi wa habari na wageni waalikwa (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam.
IMG_7921
Warembo wakipozi na kuonyesha simu ya Huawei P8  ambayo itaanza kupatikana katika soko la Tanzania kuanzia leo na itakuwa inauzwa kwa gharama nafuu ya shillingi 1,100,000 kwa simu inayotumia laini 1 na shillingi 1,200,000/- kwa simu inayotumia laini mbili.
IMG_7955
Mpiga picha wa gazeti la Serikali la Habari Leo, Mroki Mroki almaarufu kama Father Kidevu (kulia) akithibitisha ubora wa simu ya Huawei P8 wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa simu hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Huawei Tanzania, Bw.Samson Majwala.
 *************
BAADA ya kufanyika uzinduzi mkubwa wa simu ya Huawei P8 mjini Johannesburg hivi karibuni, kampuni  hiyo nguli katika sekta ya teknolojia  ya mawasiliano ya Huawei, leo hii imezindua simu  mpya ya P8  jijini Dar es Salaam ikiwa ni muendelezo wa kampuni hiyo kuleta mapinduzi kwenye nyanja ya mawasiliano ulimwenguni.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa simu hiyo leo kwa waandishi wa habari na wageni waalikwa katika hafla iliyofanyika katika hoteli ya Hyatt  Kilimanjaro jijini Dar es Salaam, Mkurungezi wa Masoko na Mauzo wa Huawei Tanzania Bwana Samson Majwala alisema uundwaji wa simu hiyo umelenga kurahisisha zaidi mahitaji ya teknolojia ya mawasiliano kwa watumiaji wa simu za kisasa zilizotengenezwa kutosheleza mahitaji mbalimbali ya wateja mbali na kutumika katika mawasiliano.

Alisema simu hii ya P8 itaanza kupatikana katika soko la Tanzania kuanzia leo na itakuwa inauzwa kwa gharama nafuu ya shillingi 1,100,000 kwa simu inayotumia laini 1 na shillingi 1,200,000/- kwa simu inayotumia laini mbili“Na hiyo ndiyo sababu kila mfumo wa simu hii upo kisasa zaidi kuanzia muonekano wake ambao kiukweli ni ‘bapa’ kurahisisha ushikwaji wake, rangi zake zenye mvuto sambamba na  kamera yenye uwezo wa hali ya juu yenye kukidhi kiu ya kiubunifu kwa kila mtumiaji wake,’’ alifafanua.

Kwa mujibu wa Bwana Majwala, simu hiyo ya P8 ambayo inaingia sokoni ikiwa na rangi tofauti nne za dhahabu, nyeusi, fedha na kijivu imeboreshwa zaidi ikiwemo kwenye mfumo wake wa ‘kutafutwa kwa sauti’, alisema.

 Akizungumzia ubora wa betri ya simu hiyo Bwana Majwala alisisitiza kwamba mfumo wa simu hiyo imezingatia matumizi ya muda mrefu kwa mfano mtumiaji  anaweza kutumia  simu kwa siku nzima bila kuiongezea umeme huku kwa wale watumiaji wa kawaida anaweza kuitumia kwa siku moja na nusu. “Mapinduzi mengine kwenye simu hii yanajidhihirisha kwenye mfumo wake wa kamera ya kupiga picha na kurekodi video  ambavyo vimeboreshwa zaidi hususani katika uchukuaji wa picha.

Sifa nyingine ya pekee katika simu hii mpya ya P8 ni kuwa na uwezo wa kuongezeka sauti kuwa kubwa kwa kiwango cha asilimia 58 zaidi ya kiwango cha kawaida iwapo mtumiaji anakuwa kwenye sehemu zenye kelele na kuwa rahisi kwake kuendelea kupata mawasiliano na haina mawimbi endapo mtumiaji anaitumia kwa kutumia waya maalumu wa kusikilizia simu masikioni au unapotumia kipaza sauti kimoja cha simu bila kusahau kudumu na chaji ya betri kwa muda mrefu.

Pia simu hii mpya mbali na kuwa na mambo mengi ya kisasa na yanayoleta furaha kwa mtumiaji inaouwezo wa kuifadhi kiasi kikubwa cha kumbukumbu kufikia 16GB au 64GB na ikiunganishwa na  interneti inakuwa na kasi ya ajabu katika kupakua data uwezo wake ukiwa zaidi ya mara tatu  ya uwezo wa simu zilizotengenezwa na makampuni mengine zilizopo kwenye masoko hivi sasa na inao uwezo wa kudaka mawasiliano na kusikika vizuri hata iwapo mtumiaji anasafiri kwa kutumia treni iendayo kasi kwa mwendo wa kilometa 300 kwa saa.
Posted by MROKI On Wednesday, July 15, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo