Nafasi Ya Matangazo

July 15, 2015




BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imeongeza muda wa waombaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016 kuwasilisha maombi yao hadi mwishoni mwa mwezi huu.

Taarifa iliyotolewa jana na HELSB nanakusainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa wake, George Nyatega, imesema hiyo ni kutoa fursa kwa wombaji ambao hawajakamilisha kufanya hivyo.
 “Hatua hii imechukuliwa ili kuwapa fursa wale ambao kwa sababu mbalimbali hawakuweza kufanya maombi ya mikopo katika  muda uliopangwa,” ilisema sehemu ya tarifa hiyo.

Awali Bodi ilianza kupokea maombi ya mikopo kupitia mtandao wake wa kwa www.olas.heslb.go.tz tamngu mwanzoni mwa mwezi Mei mwaka huu na mwisho wa maombi hayo ulipangwa kuwa Juni 30 mwaka huu.

Kupitia taarifa hiyo, HESLB imewataka waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016 ambao hawajakamilisha maombi yao kukamilisha na kuwasilisha maombi yao ya mikopo ndani ya muda ulioongezwa na kusisitiza kuwa hakutakuwa na muda mwingine wa nyongeza baada ya tarehe 31 Julai, 2015.

HESLB ilianzishwa kwa sheria ya Bunge na 9 ya mwaka 2004 na kuanza kazi rasmi mwezi Julai, 2005 ili, pamoja na majukumu mengine kutoa mikopo kwa wanafunzi wahitaji waliodahiliwa katika taasisi za elimu ya juu.



 IMETOLEWA NA:
MKURUGENZI MTENDAJI
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
Posted by MROKI On Wednesday, July 15, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo