Nafasi Ya Matangazo

February 04, 2015

Meneja Usambazaji na Matawi, Bi. Masala Korosso wa FNB Tanzania akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa matawi mapya ya benki hiyo yaliyofunguliwa Sinza Kijiweni na Mbagala Zakhem kwa lengo kusogeza huduma kwa wateja pamoja na kuhudumia biashara ndogo na za kati zinazokua kwa kasi katika maeneo hayo. Kushoto ni Meneja Huduma za Rejareja wa Benki hiyo Emmanuel Mongella
Meneja Huduma za Rejareja wa FNB Tanzania Emmanuel Mongella Meneja Usambazaji akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa matawi mapya ya benki hiyo yaliyofunguliwa Sinza Kijiweni na Mbagala Zakhem kwa lengo kusogeza huduma kwa wateja pamoja na kuhudumia biashara ndogo na za kati zinazokua kwa kasi katika maeneo hayo. Kushoto ni Meneja Matawi, Bi. Masala Korosso.
**************
 First National Bank imeongeza huduma zake kwa maeneo mengi zaidi ya jiji la Dar es salaam kwa kufungua matawi mawili mapya katika maeneo ya Sinza na Mbagala. Hii inaifanya benki hiyo kuwa na jumla ya matawi saba yaliyofunguliwa katika kipindi cha miaka mitatu. 

Meneja wa Huduma za Rejareja wa First National Bank, Emmanuel Mongella amesema kuwa matawi mapya yatakidhi mahitaji ya huduma za kibenki kutoka benki hiyo ambayo yanaendelea kuongezeka na matawi haya yatahudumia wateja wa reja reja na wateja wa biashara katika maeneo haya ambayo yana biashara ndogo na za kati zinazokua kwa kasi sana. Matawi haya yanakuja na huduma  zilizolenga kukidhi mahitaji mbalimbali ya wateja na jumuiya za biashara katika maeneo hayo. 

"Tuna imani kuwa matawi haya yatafanikiwa na tuna mipango kabambe ya kufungua matawi kwenye maeneo mengine tukianza na Arusha na Mwanza kabla ya mwisho wa mwaka huu,” alisema Mongella.

Meneja Usambazaji na Matawi, Masala Korosso alisistiza kwamba benki imechagua kuwekeza katika maeneo haya kutokana na ukuaji kasi wa jiji la Dar es salaam na kuongeza kuwa tawi  la Sinza liko eneo la Kijiweni na tawi la Mbagala liko eneo la Rangi Tatu.

Alisema kuwa Sinza na Mbagala ni maeneo muhimu kuwekeza na ndio maana FNB imeona ni wakati muafaka kuanzisha huduma zake kwenye maeneo hayo. “Kwa pamoja Sinza na Mbagala ni maeneo ambayo yanakua sana kiuchumi na hii imetulazimu kuhakikisha uwepo wa FNB katika maeneo haya”.

Ufunguzi wa matawi haya utaongeza huduma ambayo tayari inatolewa na FNB kupiti tawi la Kariakoo lililoko mtaa wa Uhuru, tawi la Makao Makuu eneo la Posta, tawi la Viwandani lililopo Quality Centre, Peninsula lililopo Oysterbay na Kimweri lililopo Msasani.
Posted by MROKI On Wednesday, February 04, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo