Nafasi Ya Matangazo

August 06, 2014

Mkuu wa Morogoro Joel Bendera akipiga mpira kuashiria uzinduzi wa Airtel Rising Stars mkoani Morogoro.
 Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera akikagua timu wakati wa uzinduzi wa Airtel Rising Stars mkoani Morogoro.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera, atilia mkazo soka la vijana na kuwataka viongozi wa mpira wa miguu mkoa wa Morogoro na chama cha mpira wa miguu Tanzania kutilia mkazo program za vijana.
Kocha wa zamani wa timu ya Taifa – Taifa Stars atoa changamoto wakati akifungua mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars mkoa wa Morogoro siku ya jumanne. Alisema kuwa hakuna njia ya mkato katika maendeleo ya mpira wa miguu zaidi ya kuwekeza katika shule za soka na programu za vijana kama Airtel Rising Stars. Awapongeza  Airtel kwa mchango wao.
Zaidi ya majuma mawili kumekua na maoni ya kutoka kwa wakuu wa mikoa na wadau wengine wakisisitiza viongozi wa mpira wa miguu nchini kutilia mkazo programu za vijana kuiwezesha Tanzania kufanya vizuri.
Wakifungua mashindano ya Airtel Rising Stars katika mikoa yao hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam Said Meck Sadiki na Mkuu wa mkoa Mbeya Abbas Kandoro nao walitilia mkazo kuwekeza katika mpira wa vijana. Wengine waliotoa maoni hayo ni meya wa Mwanza Stanslaus Mabula na Mbunge wa Ukonga Eugen Mwaiposa.
Mashindano ya Airtel Rising Stars yanaitimishwa leo (August 7) na timu zinatarajiwa kuwasili jijini Dar-es-Salaam siku ya jumamosi August 9 katika fainali za taifa ambazo zinaanza kutimua vumbi jumapili katika kiwanja cha kumbukumbu ya Karume. Fainali za Taifa zitamalizika tarehe 17 August na wachezaji wakiume na wa kike watakao chaguliwa wataweka kambi jijini Dar-es-Salaam wakijiandaa na mashindano ya kimataifa Airtel Rising Stars yatakayofanyika nchini Gabon.
Mwaka jana mashindano hayo yalifanyika nchini Nigeria na timu ya wasichana ya Tanzania walinyakua ubingwa na kuzawadiwa dollar za marekani 10,000.
Posted by MROKI On Wednesday, August 06, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo