Nafasi Ya Matangazo

November 29, 2013


Wateja wa Skylight Band wiki iliyopita walipata nafasi ya kuburudika na kinywaji kipya kabisa toka nchini Sweden MOKAI Cult ambacho kina Alcohol 4.5 yenye ladha murua kama aina ya Savanna ambacho ni zaidi ya Savanna.

Hakika wateja wa Skylight Band katika ukumbi wa Thai village Masaki wiki iliyopita walichangamka kweli na kinywaji hiki toka huko Sweden chenye Alchohol ya wastani ambayo mtu anaweza kumudu kunywa na kuamka safi kabisa bila Hang-Over.
 DSC_0412
Mashabiki wa Skylight Band wakiingia getini walipata fursa ya kuonjeshwa kinywaji hicho kipya kutoka Sweden kinachotambulika kama MOKAI Cult ambacho kitakuwepo kila siku ya Ijumaa ndani ya Thai Village jijini Dar na kuzidi kuwachangamsha mashabiki wa Bendi hiyo kusakata Rhumba zaidi.
IMG_5171
Mrembo wa MOKAI Cult akifafanua jambo kwa wateja juu ya kinywaji hicho kipya.
IMG_5164
Mbunifu wa Mavazi Gabriel Mollel akiuza sura na Models Neema Mbuya pamoja na Anna.
IMG_5181
Miss Tanzania 2011 Salha Israel (wa tatu kulia) kwenye picha ya pamoja na marafiki zake ndani ya Thai Village-Masaki jijini Dar Juma lililopita.
DSC_0393
Pichani juu na chini ni mashabiki wa Skylight Band wakipata Ukodak na Warembo wa MOKAI Cult waliokuwa wakaribu kwa wateja na kutoa huduma yenye kiwango cha kimataifa. Njoo wewe na yule leo tujikoki na MOKAI.
DSC_0418 DSC_0431 IMG_5141
Rappa wa Skylight Band Joniko Flower akiongoza makamuzi na kikosi kazi cha band hiyo kutoa burudani kwa mashabiki wake Ijumaa iliyopita ndani ya ukumbi wa Thai Village jijini Dar.
IMG_5187
Divas wa Skylight Band wakiongozwa na Aneth Kushaba AK47 katika burudani ya aina yake yenye kiwango cha kimataifa kwa mashabiki wake. 
Picha zaidi: MO BLOG
Posted by MROKI On Friday, November 29, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo