Nafasi Ya Matangazo

October 17, 2013

 Muuguzi wa Hospitali ya Tanwat, Asnath Mdakule akitoa huduma ya upimaji wa afya ya magonjwa ya shinikizo la damu ‘BP’ na uwiano kati ya urefu na uzito kwa mmoja wa wananchi waliotembelea banda la Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), wakati maonesho ya uzinduzi wa mkoa mpya wa Njombe, ikiwa ni moja ya huduma zinazotolewa na shirika hilo katika mafao ya Matibabu. (Picha na Shaban Lupimo)
 Muajiri Mkubwa wa NSSF Njombe ambae ni  Mhandisi wa kampuni ya Tanwat Njombe Umesh Radd akisaini kitabu cha wageni kabla ya kupokea maelezo kuhusiana na uanachama wa hiari na sekta binafsi kutoka  kwa Meneja wa Shirika la Hifadhi ya Jamii NSSF mkoa wa Njombe, Godwin Mwakalukwa baada ya kutembelea banda la shirika hilo kwenye maonesho ya uzinduzi wa mkoa katika uwanja wa. 
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Kapteni Mstaafu Aseri Msangi (kushoto) akipokea maelezo kuhusiana na uanachama wa hiari na sekta binafsi kutoka  kwa Meneja wa Shirika la Hifadhi ya Jamii NSSF mkoa wa Njombe,Godwin Mwakalukwa (katika) baada ya kutembelea banda la shirika hilo kwenye maonesho ya uzinduzi wa mkoa katika uwanja wa SabaSaba kulia ni Ofisa Uhusiano wa shirika hilo Maife Kapinga. 

Posted by MROKI On Thursday, October 17, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo