Nafasi Ya Matangazo

September 30, 2013

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu,Uwekezaji na Uwezeshaji,Dk Mary Nagu(kushoto)akitambulishwa Viongozi mbalimbali wa International Association of  Public Health Institutes(IANPHI)katika hoteli ya Ngurdoto Mountain,Arusha leo na Makamu wa Rais wa taasisi hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa National Institute for Medical Research(NIMR)

Kundi maarufu la Tanzania House of Talent(T.H.T)kutoka jijini Dar es Saalam likitoa burudani katika mkutano ulioanza leo jijini Arusha.

Makamu Mwenyekili wa taasisi ya  International Association of  Public Health Institutes(IANPHI) ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa National Institute for Medical Research(NIMR)Dk Mwelesele Malecela akitoa hotuba yake mapema leo kwenye mkutano unaofanyika katika hoteli ya Ngurdoto Mountain Arusha.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu,Uwekezaji na Uwezeshaji,Dk Mary Nagu ambaye alikua mgeni rasmi akifungua mkutano wa nane wa taasisi ya  International Association of  Public Health Institutes(IANPHI)katika hoteli ya Ngurdoto Mountain,Arusha leo ambao lengo lake ni kuona nafasi ya taasisi hiyo baada ya mwaka 2015.

Baadhi ya madaktari kutoka mataifa mbalimbali wakiwa kwenye mkutano huo.

Rais wa taasisi ya International Assocition of Public Health Institutes,Profesa Pekka Puska akimwachia Njiwa ndege anayeashiria amani .

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu,Uwekezaji na Uwezeshaji,Dk Mary Nagu(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa afya  kutoka mataifa mbalimbali ulimwenguni baada ya kufungua mkutano wa nane wa taasisi ya  International Association of  Public Health Institutes(IANPHI)katika hoteli ya Ngurdoto Mountain,Arusha leo.

Na Mwandishi Wetu,Arusha
Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu,Uwezeshaji na Uwekezaji,Dk Mary Nagu amezitaka taasisi za afya ya jamii kukabiliana na changamoto za kiafya za magonjwa yanayoambukizwa na yasiyoambukizwa ili kuwa na jamii yenye afya njema wanaweza kuongeza tija.

Ametoa kauli hiyo leo wakati akufungua mkutano wa nane unaojadili nafasi ya taasisi hiyo baada ya kikomo cha malengo ya Millenia ifikapo mwaka 2015 na kuwataka vijana kujiepusha na ugonjwa hatari wa Ukimwi.

Mkurugenzi wa taasisi ya Utafiti wa magonjwa ya binadamu nchini(Nimr)amesema mkutano huo ni wa kipekee na wa kwanza kufanyika katika nchi za Afrika Mashariki na wa pili barani Afrika utaojadili mada mbalimbali zinazohusu magonjwa yanayoambukizwa na yasiyo ya kuambukizwa.

Amesema magonjwa yanayoambukizwa katika nchi zilizoendelea yamepungua ukilinganisha na nchi zinazoendelea huku mkazo mkubwa ukihitajika kuongezwa kwa magonjwa yasiyoambukizwa ambayo kwa sehemu kubwa huchangiwa na tabia za maisha ya kila siku. 

Posted by MROKI On Monday, September 30, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo