Nafasi Ya Matangazo

August 13, 2013

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Montage Tanzania Teddy Mapunda  akiwagawia soda wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya watoto wa kike  ambao ni yatima na wanaoishi  katika mazingira hatarishi ya WAMA-Nakayama iliyopo kijiji cha Nyamisati wilaya ya Rufiji mkoani Pwani wakati wa sherehe za sikuku ya Eid Mubarak zilizofanyika shuleni hapo jana. Wafanyakazi wa kampuni hiyo  walisherehekea sikuu hiyo na  wanafunzi hao ili kuonyesha upendo.
Katibu wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Daud Nasibu akiongea na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya watoto wa kike  ambao ni yatima na wanaoishi  katika mazingira hatarishi ya WAMA-Nakayama inayomilikiwa na taasisi hiyo wakati wa sherehe za Eid Mubarak ziliyofanyika shuleni hapo jana.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Montage ya jijini Dar es Salaam  wakiwahudumia chakula cha mchana wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya watoto wa kike  ambao ni yatima na wanaoishi  katika mazingira hatarishi ya WAMA-Nakayama iliyopo kijiji cha Nyamisati wilaya ya Rufiji mkoani Pwani. Wafanyakazi wa kampuni hiyo waliamua kusherehekea sikukuu ya Eid Mubarak na wanafunzi hao jana  ili kuonyesha upendo
Wanafunzi  wa Shule ya Sekondari ya watoto wa kike  ambao ni yatima na wanaoishi  katika mazingira hatarishi ya WAMA-Nakayama iliyopo kijiji cha Nyamisati wilaya ya Rufiji mkoani Pwani wakila chakula cha mchana kilichoandaliwa na kampuni ya Montage Tanzania wakati wa sherehe za Eid Mubarak zilizofanyika shuleni hapo jana.
Baadhi ya wanafunzi  wa Shule ya Sekondari ya watoto wa kike  ambao ni yatima na wanaoishi  katika mazingira hatarishi ya WAMA-Nakayama iliyopo kijiji cha Nyamisati wilaya ya Rufiji mkoani Pwani wakicheza mziki aina ya Kwaito  jana wakati wa sherehe za  Eid Mubarak zilizofanyika shuleni hapo.
Posted by MROKI On Tuesday, August 13, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo