Nafasi Ya Matangazo

August 14, 2013

UTANGULIZI
Mfuko wa Pensheni wa PPF  ni Mfuko mkongwe hapa nchini, ulianzishwa mwaka 1978 kwa Sheria ya Mfuko wa Pensheni wa PPF Sura na. 372 kwa madhumuni ya kutoa mafao ya pensheni na mafao mengine yanayoendena na hayo kwa wafanyakazi wote walio katika sekta rasmi na zisizo rasmi.

majukumu ya mfuko

PPF ina majukumu yafuatayo:-
kuandikisha wanachama,
kukusanya michango,
kuwekeza michango inayokusanywa na
kulipa mafao ya pensheni na mafao mengine yanayoendana na hayo kwa wanachama wake.

WIGO WA UANACHAMA
Mfuko unaandikisha wanachama kutoka katika sekta zote za uchumi mashirika ya umma, makampuni binafsi, waliojiajiri wenyewe na sekta isiyo rasmi

Mafao ya PPF: Mfuko wa PPF una mafao saba baadhi ya mafao ambayo Mfuko unatoa ni
Mafao ya Pensheni ambapo hutolewa pale ambapo mwanachama anapokuwa amechangia kwa kipindi cha miaka 10 au zaidi na amefikia umri kustaafu yaani miaka 55 mpaka 60.Na awe ameondoka kwenye ajira.


Mpaka sasa PPF ina wastaafu  wapatao 25,896 na tunalipa kila mwezi Billioni 3.7
Hii ni kwa mafao ya uzeeni tu mnaweza kuona jinsi tunavyosaidia kuondoa umaskini na kukuza uchumi wa nchi.

Mafao ya Ugonjwa
 Hutolewa pale ambapo mwanachama wa PPF anapokuwa ameondoka kazini kwa sababu za ugonjwa na imedhibitishwa na Daktari kwamba kweli hawezi kufanya kazi tena

Mafao ya Elimu:
Hutolewa pale ambapo mwanachama wa PPF anapokuwa amefariki dunia baada ya kuchangia kwa muda wa miaka 3 au zaidi.

Fao hili hutolewa kwa watoto wa mwanachama wasiozidi 4 kwa kulipia gharama ya elimu ya chekechea mpaka kidato cha nne.

Kwa kutambua umuhimu wa elimu kuanzia mwakani 2014 Mfuko unaongeza muda wa kuwasomesha watoto mpaka kidato cha sita.
Tunalipa mmoja kwa mmoja kwenye shule za watoto wanachama

UWEKEZAJI
Jukumu linginge kubwa ni kuwekeza; Mfuko wa PPF unawekeza kwa mujibu wa sera ya uwekezaji sambamba na mwongozo wa uwekezaji wa SSRA na BOT.  Baadhi ya sehemu Mfuko unawekeza katika Majengo kama vile ofisi mfano PPF Tower,PPF Plaza Mwanza,vile vile wekeza kwenye hoteli,nyumba za kupanga vile vile tume tumeshiriki kwenye ujenzi wa vyuo vikuu kama vile UDOM-kwenye chuo cha Mifumo ya Komputa na chuo kikuu cha sayansi na Teknologia Nelson Mandela kilichopo Mkoani Arusha.

Tumeshiriki kwenye uwekezaji katika sekta ya Kilimo Kagera Sugar, 21st Century kiwanda cha Nguo Morogoro Uwekezaji mwingine ni kwenye Mikopo ya Saccos kwa wanachama wetu ambapo PPF unakopesha wanachama kwenye maeneo ya Kazi ambapo inasaidia kukuza uchumi

MAFANIKIO YA MFUKO
Mfuko umetimiza miaka 35 mwaka huu na ulianza kwa mtaji wa shilingi million 50 mwaka 1992.lakini Mfuko unaendelea vizuri kwa kuwa na uwezo wa kulipa mafao kwa wakati bila kulazimika kuuza vitega uchumi au kukopa mahali popote

Kwa upande wa thamani ya Mfuko:
Mfuko umeendelea kukua mwaka hadi mwaka ambapo kwa sasa thamani ya Mfuko ni shilingi trillion 1.3 ukilinganisha na mwaka jana 2012 Desemba ambapo thamani ya Mfuko ilikuwa trillion 1.09

IDADI YA WANACHAMA
Mfuko umeendelea kukua kwa upande wa uanachama ambapo hadi kufikia mwezi Juni 2013, tulikuwa na jumla ya wanachama 224,193 ukilinganisha na wanachama 203,981 kwa mwezi Desemba 2012

Matumizi ya mifumo ya habari:
Mfuko umefanikiwa sana katika nyanja ya teknolojia kwa kuweza kulipa mafao kwa kutumia mtandao, hivyo kulipa kwa wakati.

Vile vile Mfuko umepunguza matumizi ya karatasi yaani ‘paper work’ kwa kurahisisha malipo kwa wanachama na kwa upande wa watoa huduma tunatumia  mfumo wa ‘E-banking’ yaani pesa zinatumwa moja kwa moja kwenye akaunti ya mhusika.

Kupitia mifumo ya kisasa ya PPF, mwanachama anaweza kupata taarifa zake za michango, dai au pensheni kwa mstaafu kupitia simu ya kiganjani au tovuti ya Mfuko ambayo ni www.ppftz.org
Mwanachama anaandika neno michango anaacha nafasi anaweka namba ya   uanachama na kutuma kwenye namba 15553.

Si hivyo tu , bali hata mwajiri anaweza kupata taarifa za michango ya wafanyakazi wake akiwa katika sehemu yake ya kazi bila kwenda katika ofisi za PPF hii inaokoa muda na pia kuongeza uhakika wa uwasilishwaji wa michango ya wanachama.

Kwa kutambua umuhimu wa matumizi ya mifumo ya habari mwaka huu 2013 katika wiki ya Hifadhi ya Jamii, Mfuko wa Pensheni wa PPF ulitunukiwa hati ya  utambuzi kama Mfuko bora kwenye matumizi ya Mifumo ya habari. Hati hiyo ilitolewa na Mhe. Rais, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete,kwa kuwa Mfuko bora katika Nyanja ya mifumo ya habari kwa kutumia teknolojia ya kisasa kwenye kutoa huduma mbalimbali.

Utoaji wa Mikopo ya SACCOS
PPF ni waanzilishi wa mikopo ya SACCOS tulianza kutoa mikopo ya saccos mwaka 2004.
Tunatoa mikopo hii kupitia SACCOS za wanachama wetu zilizopo kwenye maeneo yao ya kazi.
Mpaka sasa tumeshatoa zaidi ya Billioni 56 kwenye SACCOS 46

Tuzo katika Utawala bora
Kwa kutambua uwazi katika uendeshaji wa Mfuko Umoja Mifuko ya hifadhi ya Jamii Duniani (issa) uliweza kutupatia Tuzo katika utawala bora kwa kuendesha shughuli mbali mbali kwa uwazi kama vile mikutano ya wanachama na wadau PPF huu ni mwaka wa 23 tuna desturi ya kukutana na wanachama na wadau wetu.
Hati safi kutoka kwa CAG kwa kuwa na mahesabu yaliyo safi
Uwekezaji ni mzuri ambapo tumewekeza katika sehemu mbalimbali kama vile hoteli za kitalii mfano East African Hotel Arusha na Gold Crest Mwanza ambapo watalii wengi wanafika hivyo inasaidia kwenye ukuaji wa Uchumi.

Tumewekeza kwenye ujenzi wa nyumba za bei nafuu kwa ajili ya kuwauzia wanachama wetu.PPF imekuwa Mfuko wa kwanza kwa kuanzisha miradi ya nyumba za bei nafuu.
Tulijenga nyumba 580 Kiseke Mwanza na tuliziuza kwa bei nafuu ya kati ya  shilingi millioni 16 mpaka million 33. Zoezi hili ni endelevu kwa mikoa mingine

Fao la Elimu:
PPF imekuwa Mfuko wa kwanza kuwa na Fao la elimu kwa watoto wa wanachama wetu.Ambapo lilianza kutolewa mwaka 2003 ambapo tangu tuanze kwasomesha kiasi cha shilingi billion 3.6

LENGO
Katika Mpango mkakati wa Mfuko kwa kipindi cha miaka 3 (2013-2015) baadhi ya malengo ya Mfuko ni kama ifuatavyo:
Thamani ya Mfuko ni kukua kutoka trillion 1.09 Desemba 2012 na kufikia trillion 2 ifikapo  Desemba 2015 Na Idadi ya wanachama kuongezeka kutoka wanachama 203,981 Desemba 2012 kufikia laki 4 Desemba 2015. Lengo kuongeza mara mbili thamani ya Mfuko

Mwisho kabisa ningependa kuwashukuru wanachama na wadau wote wa Mfuko kwa Mchango Mkubwa Mliotupa Hivyo tunaomba tuendelee kushirikiana kwa kuendelea kuwa wanachama wa PPF na wale ambao bado hamjajiunga na PPF tunaomba mjiunge ili muweze kuwa na uhakika wa maisha yenu ya sasa na baadaye.
Posted by MROKI On Wednesday, August 14, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo