Nafasi Ya Matangazo

August 07, 2013



Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa benki ya KCB, Christina Manyenye, akimkabidhi Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa ya Mwananyamala, Dk. Sophinias Ngonyani (kushoto), moja ya vifaa tiba vyenye thamani ya sh. milioni 7.2, vilivyotolewa na benki hiyo, vinavyotumika kwa ajili ya kumwekea gesi mgonjwa, Dar es Salaam jana. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa KCB, Godfrey Ndalahwa.




Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa ya Mwananyamala, Dk. Sophinias Ngonyani, akiangalia moja ya vifaa tiba vya kumwekea mgonjwa gesi, mara baada ya kukabidhiwa na Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa benki ya KCB, Christina Manyenye (katikati), vifaa vilivyotolewa na benki hiyo kwa hospitali hiyo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi
Mtendaji wa KCB, Godfrey Ndalahwa.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya KCB, Godfrey Ndalahwa, akimkabidhi moja ya boksi lenye vifaa vya kumwekea mgonjwa gesi, Mkuu wa Bima ya Afya wa Hospitali ya Mkoa ya Mwananyamala, Dk. Merina Nkullua, vilivyotolewa na benki hiyo, Dar es Salaam jana. Katikati ni Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa benki ya KCB, Christina Manyenye


Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa ya Mwananyamala, Dk. Sophinias Ngonyani (kushoto), akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhiwa vifaa tiba vya kuwekea mgonjwa gesi, vilivyotolewa na benki ya KCB kwa hospitali hiyo, Dar es Salaam jana. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa KCB, Godfrey Ndalahwa na katikati ni Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa benki ya KCB, Christina Manyenye.
Posted by MROKI On Wednesday, August 07, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo