Nafasi Ya Matangazo

July 25, 2013

 

 Afisa Mtendaji mkuu wa TTCL Dtk. Kamugisha Kazaura  akibadilishana mawazo na Kiongozi wa ujumbe kutoka ubalozi wa Marekani  hapa nchini Bw. Jeff            Shrader.
 Kiongozi wa ujumbe kutoka ubalozi wa Marekani hapa nchini Bw.  Jeff Shrader akitoa shukrani zake kwa uongozi na wafanyakazi wa TTCL  alipotembelea makao makuu ya Kampuni hiyo.
 Afisa Mkuu wa Mauzo na Masoko wa TTCL Bw. Peter Ngota  akiwashukuru wawakilishi kutoka ubalozi wa Marekani hapa nchini kwa  kutambua mchango wa TTCL katika kufanikisha ziara ya Rais wa  Marekani alipotembelea Nchini Tanzania.
 Uongozi wa TTCL pamoja na wawakilishi wa Ubalozi wa Marekani  hapa nchini katika picha ya pamoja.
Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL dkt. Kamugisha Kazaura akipokea  cheti cha shukrani kutoka kwa Kiongozi wa ujumbe kutoka ubalozi wa  Marekani hapa nchini Bw. Jeff Shrader.
*******
Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) imepongezwa na Ubalozi wa Marekani  kwa huduma bora iliyotoa  wakati wa ujio wa Rais wa Marekani hapa nchini.
Akitoa shukrani hizo Kiongozi wa ujumbe kutoka  ubalozi wa Marekani  hapa nchini Bw. Jeff Shrader  amesema, Ubalozi wa Marekani Nchini Tanzania umejipatia sifa kubwa kwa huduma bora na za uhakika  kutoka TTCL wakati wote wa ujio na uwepo wa Rais wa Marekeni hapa nchini.
Ameongeza kuwa huduma walizozipata  zimethibitishwa na taarifa kutoka ofisi inayoratibu safari za Rais wa Marekani kuwa katika nchi walizopita Afrika huduma ya mawasiliano ialiyoipata Tanzania ilikuwa ni ya kiwango cha juu na aliipongeza TTCL na kusema hii ni sifa kubwa kwa Serikali ya Tanzania na Ubalozi wa Marekani hapa nchini.
 
Akipokea salam hizo za shukrani kutoka kwa ujumbe huo wa Marekani, Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Dkt. Kamugisha Kazaura  amesema, TTCL ilifanya kazi yake kwa uhakika na ina uwezo wa kuhimili mahitaji ya watanzania na Kimataifa pia.
 
Ameongeza kuwa TTCL inaendelea na juhudi za kujikita zaidi katika huduma ya data/ intanet na kuendelea kuboresha gharama ili kila mtanzania apate fursa ya kunufaika na mawasiliano ya simu pamoja na data.
Katika Shukurani zake Bw. Jeff Shrader alioa pia zawadi kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Dkt. Kamugisha Kazaura  na kwa baadhi ya wawakilishi kutoa fani mbalimbali za Ufundi na Biashara kwa niaba ya wafanyakazi wote wa TTCL kama ishara yao ya shukurani kwa TTCL na Taifa kwa ujumla.
Posted by MROKI On Thursday, July 25, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo