Nafasi Ya Matangazo

March 18, 2013



Mahmoud Ahmad Arusha
Wakazi wa jiji la Arusha leo wameonja joto ya jiwe na adha ya mgomo wa usafiri wa dala dala ukihusishwa na masuala ya rushwa na kisiasa yanayoendelea kwenye jiji hili huku wananchi wakitembea umbali wa takribani kilometa 6 kwa miguu kufika katikati ya jiji hili.

Mgomo huo ulioanza tangia Alfajiri hadi saa tisa mchana uliacha shughuli za kimaendeleo kusuasua kwa muda huku wakazi wa maeneo ya Mbauda,ffu,kwa Morombo,na kisongo wakionja joto ya jiwe kutokana na mgomo huo.

Suala la rushwa kwa askari wa jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani na suala la kisiasa yamehusishwa moja kwa moja na mgomo huo ambapo baadhi ya madereva na makondakta waliohojiwa na wanahabari wamesema kuwa askari wamakuwa wakiwatuma chips kuku kila wanapowakamata.

Madai hayo yalienda sambamba na madai yaliyotolewa yakimuhusu mwanasiasa moja jijini hapa kuwahamasisha madereva hao kugoma kwa masuala yake ya kisiasa na huku madereva hao wakilaumu jeshi la polisi kuwakamata kwa siku hadi mara tano hali inayoleta usumbufu kwa madereva hao kukosa posho zao za kila siku

“utakuita trafiki anakutuma chips kuku na saingine anakwambia utupie buku jero huku ni kuumizana kwani inakuwa tunawafanyi kazi wao na familia zao huku tukitoa malalamiko yetu kwa mkubwa wao yamekuwa yakiishia hewani sasa leo tumeamua kugoma”alisema moja wa madereva hao wa mbauda


Akizungumza na waandishi wa habari mkuu wa wilaya ya Arusha John Mongela alisema kuwa hakuna aliyejuu ya sheria na kuwa yeyote atakayebainika kuchochea vurugu hizo zilizoenda sanjari na mgomo hatua kali za kisheria zitafuata mkondo wake na kuwa hawatafumbia macho wale wote wanaotumia makundi kuwathiri wananchi kwa manufaa yao ya kutaka umaarufu.

Alisema kuwa wameunda kamati ya muda kutatua masuala yote ya usafiri wa daladala almaarufu Vifodi jijini hapa na kuwa hawatangoja hadi mgomo utokee tena kwani kila mwezi watakuwa wakikutana kupeana taarifa na matukio mbali mbali iliwaweze kuyatatua kwa wakati.

“unajua mgomo huu usitumiwe na wanasiasa kutaka kujipatia umaarufu kwani wamakuwa wakiwashaiwishi vijana kufanya matendo ya siyo ya kiustaarabu anaakibainika mwanasiasa yeyote kuwa waliwashawishi vijana kuwazuia madereva kuendesha mgomo huo hatutasita kuchuwa hatua kali za kisheria dhidi yake hatutamuogopa mtu kwenye hili”alisema Mongela

Mgomo wa vifodi jijini hapa umekuwa ukihusishwa na mambo ya kisiasa kwa kila mara jeshi la polis mkoani hapa linapozuia maandamano ya chama kimoja cha siasa wamekuwa wakitumia vijana kuwadhibiti madereva wa vifodi kutoendesha kazi zao huku wakitoa vitisho na saa ingine kuwapiga madereva wanaokaidi amri yao

Wananchi kadhaa waliohojiwa wameitupia lawama za moja kwa moja mamlaka husika kwa kufumbia macho vitendo vya vijana hao waliokuwa wakizuia magari kuingia jijini hapa kwa madai kuwa wametumwa kutoka ngazi za juu.

Posted by MROKI On Monday, March 18, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo