Nafasi Ya Matangazo

March 18, 2013




Evelyn Mkokoi,Afisa Habari Ofisi ya Makamu wa Rais
Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira dkt Terezya Huvisa, amezingua moja ya miradi wa maji safi na salama, katika kijiji cha Ng’mbo wilaya mpya ya Nyasa katika mkoa wa Ruvuma ikiwa ni njia mojawapo ya kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi.

Akizindua kisima hicho, Dkt Hufisa alieleza kuwa, mradi huo wa maji safi na salama kwa matumizi ya binadamu katika kijiji hicho umewalenga zaidi wanawake kwani wao wamekuwa wakitumia muda mwingi kwenda kutafuta maji ziwani au katika visima vya muda kwa matumizi ya nyumbani,hivyo kisima hicho kitawasaidi kuokoa muda na kushiriki katika shughuli nyingine za kimaendeleo.

Dkt Hufisa aliongeza kwa kusema kuwa, wananchi wana haja na kila sababu ya kupata elimu ya kutosha juu ya utunzaji wa vyanzo vya maji na mazingira, na halmashauri iweke mikakati ya kutunza vyanzo vya maji pamoja na kupanda miti na kuitunza.


Aidha dkt Huvisa amewaasa wananchi kushirikiana na police jamii wanaosimamia masuala ya mazingira katika kubaini waharibifu wa mazingira wanaovua kwa kutumia nyavu na uvuvi haramu.

Awali  mratibu wa kitaifa wa mradi huo kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira bw. Faraja Ngeregeza ameeleza kuwa, lengo la mradi huo ni kujengea uwezo wananchi na wanakijiji ili kuweza kuhimili athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi hasa zinazotokana na upungufu wa maji safi na salama.

Bw. Faraja alisema kuwa kijiji cha Ng’ombo hakikuwa na maji safi na salama kwa muda mrefu hali iliyowalazimu wanakijiji hichohususan kina mama kutembea muda mrefu kutafuta maji kwa matumizi ya nyumbani. “kukamilika kwa mradi huu kumetoa fursa kwa kina mama kupata maji kwa muda mfupi na kupata muda wa kushiriki katika shughuli nyinine za kimaendele.”alisisitiza.

Mradi huu unaotekelezwa na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira unafadhiliwa na serikali ya japan kupitia shirika la maendeleleo la umoja wa mataifa unatarajia kukamilisha ujenzi wa visima vingine katika wilaya ya misenyi mkoani Kagera,Igunga mkoani Tabora na maeneo ya Nungwi mjini Zanzibar ikiwa ni kwa ajili ya kuhimili athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.

Posted by MROKI On Monday, March 18, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo