Nafasi Ya Matangazo

December 10, 2012

Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Masoko wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa, akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya kutangaza udhamini wa kampuni hiyo katika Mbio za Kili Marathon kwa Mwaka huu, Vodacom imedhamini Mbio za kilomita 5 za Fun run ikiwa ni Mara ya sita mfurulizo. Pamoja nae ni Mratibu wa mashindano hayo Angela Damas.
 *******
Vodacom yadhamini mbio za Vodacom 5km Fun Run kwa mara ya sita
10/12/2012 Kwa mara nyingine tena Vodacom Tanzania inadhamini mbio za kujifurahisha za Vodacom 5km Fun Run ambazo ni sehemu ya mbio za Kilimanjaro Marathon zinatarajiwa kufanyika tarehe 3 Machi 2013 huko Moshi. Hii ni mara ya sita kwa Vodacom kudhamini mbio hizi. 

Akiongea na waandishi wa habari kwenye hafla ya kutangaza uzinduzi huo, Mkuu wa Mawasiliano wa Vodacom, Kelvin Twissa alisema: “Tumeamua kudhamini tukio hili kwa sababu linawaleta pamoja watu kutoka nyanja mbalimbali katika maisha.

 Vodacom 5km Fun Run ipo kwa ajili ya kutoa fursa kwa watu wa umri na makundi mbalimbali kushiriki katika mbio hizi za kimataifa na kuzidi kuifanya Kilimanjaro Marathon kuwa tukio linalohusisha watu wote.”

“Tuna shauku kubwa kuweza kuwa sehemu ya Kilimanjaro Marathon tukio ambalo hivi sasa ni kati ya matukio makubwa kabisa ya kimichezo hapa Tanzania na katika Ukanda wa Afrika Mashariki. 

Tukio hili linavutia maelfu ya washiriki kutoka ndani na nje ya nchi. Vilevile ni muhimu kusema kwamba tukio hili limeweza kuvuta hisia za wapenzi wa mbio ndefu duniani”. 

Tangu tulivyodhamini tukio hili kwa mara ya kwanza mwaka 2008, tumeshuhudia mbio hizi zikikua kwa kasi ya aina yake na tumefurahishwa na fursa ya kuendelea kuwa sehemu ya Kilimanjaro Marathon ambapo tuna nafasi ya kuwaunga mkono wanariadha wetu katika tukio hili la kimataifa kimichezo,” aliongeza. 

Vodacom itahakikisha kuwa kila mtu anakuwa sehemu ya shamrashamra za siku hiyo kwani maana itatoa fursa kwa wanaotaka kutembea, kukimbia na hata kutambaa kila mmoja kwa mwendo wake kushiriki. 

Mbali na udhamini wa mbio hizo za kujifurahisha, Vodacom pia itahakikisha waandaaji wa mbio hizo wanakuwa na mawasiliano ya uhakika kwa kuwapa namba maalum za simu pamoja na muda wa maongezi.

Ikiwa ni sehemu ya ushiriki wetu kwenye Kilimanjaro Marathon, tutaleta wafanyakazi wetu kushiriki kwenye Kilimanjaro Marathon Corporate Challenge na vilevile taasisi yetu ya Vodacom Foundation itatumia tukio hilo kusaidia jamii katika Mkoa wa Kilimanjaro kwa sababu tunaamini katika kuleta mabadiliko na kuboresha maisha ya Watanzania wote.
Posted by MROKI On Monday, December 10, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo