Nafasi Ya Matangazo

December 13, 2012

A
Tukio hilo limetokea kijijini hapo siku ya Alhamis tarehe 06/12/2012 majira ya saa sita usiku, ambapo Polisi kupitia mkakati wake wa Polisi Jamii na Ulinzi Shirikishi walipata taarifa za kuuzwa kiholela kwa Dawa mbalimbali za Binadamu katika kijiji hicho.

Uchunguzi wa awali  ulianza mara moja kuhusiana na taarifa hizo, ambapo  taarifa zilizomuhusisha mwenyekiti huyo kuhusika na biashara hiyo zilipatikana. “Wanakijiji katika eneo hilo walikiri kwamba mwenyekiti huyo amekuwa akiuza Dawa hizo  mara kwa mara.”

Mwenyekiti huyo amekuwa akifungua chumba cha kuhifadhia Dawa katika Zahanati hiyo kisha kuiba na kwenda kuziuza yeye akiwa na mshirika wake ambaye tumemkamata, amekuwa akifanya hivyo kwa kuwa yeye ndiye  mwenye Dhamana ya kutunza funguo za chumba hicho.

Aidha mshirika wake alipofanyiwa upekuzi nyumbani kwake alikutwa na makopo ya Dawa aina za Paracetamol, Piritoni na nyingine za aina mbalimbali ambazo ni miongoni mwa zilizoibwa katika zahanati hiyo, thamani ya Dawa hizo bado hazijafahamika hadi sasa.

Upelelezi unakamilishwa ili watuhumiwa hao wafikishwe mahakamani mara moja.

Natoa wito kwa wanajamii kwa kupitia mkakati wa Polisi jamii na Ulinzi Shirikishi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa mbalimbali za wahalifu na uhalifu ili kwa pamoja tuweze kuzuia na kupambana kero na matishio ya aina mbalimbali katika maeneo yetu.
Posted by MROKI On Thursday, December 13, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo