Nafasi Ya Matangazo

October 12, 2012


Pichani ni Naibu Balozi wa Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Ramadhan M. Mwinyi, akizungumza wakati wa majadiliano kuhusu ajenda ya Umalizaji Ukoloni, katika Mkutano wa Kamati ya Nne ya Baraza Kuu la 67 la Umoja wa Mataifa, Kamati hiyo ambayo ni maalum inajihusika na Masuala ya Siasa na Umalizaji wa Ukoloni 
*******
 Na  Mwandishi Maalum.
Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi, Naibu Balozi katika Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  akizungumza wakati wa mkutano wa  Kamati ya Nne ya Baraza Kuu la 67 la Umoja wa Mataifa. Kamati hiyo  ni  Kamati Maalum inayohusika na masuala ya Siasa na umalizaji wa Ukoloni na kwa wiki nzima imekuwa ikijadili  ajenda zinazohusiana na suala zima la umalizaji wa Ukoloni kama inavyoelekezwa  katika  Katiba ya Umoja wa Mataifa na Maazimio mengine mbalimbali.

Hadi sasa kuna makoloni 16 ambayo  bado yapo chini ya Ukoloni na hayajawa huru kujiamulia mambo yake yenyewe. Baadhi ya Makoloni hayo ni  Sahara ya Magharibi  ambayo ni koloni pekee lililobaki Barani Afrika.

 Kwa zaidi ya miaka 57 Sahara ya Magharibi ambayo imejitangaza kujitenga kutoka  Morocco imekuwa katika mgogoro mkubwa   na serikali ya  Morocco.  Mgogoro ambao umesababisha  wananchi wengi kupoteza maisha, wengine kuishia kuwa wakimbizi huku zikiwamo shutuma za ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

Aidha Kamati  hiyo  ilipata fursa ya   kuwasilikiliza    Wadai (Petitioners) 68 ambao ama walikuwa  wakitetea haki ya  Sahara Magharibi kujipatia uhuru wake na fursa ya kujiamulia mambo yao  au walikuwa wakiitetea Morocco dhidi ya Sahara Magharibi.

Akichangia maoni  ya  Tanzania katika mkutano huo,    Naibu Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi pamoja na  mambo mengine amesisitiza haja na umuhimu wa Serikali ya Morocco na   POLISALIO kuendelea na mazungumuzo ya kutafuta suluhu ya kudumu na kubwa zaidi ni  kwa  Morocco kuiachia  Sahara Magharibi  ijitawale na kujiamulia  mambo yake yenyewe.

Aidha  Tanzania kupitia msemaji  wake huyo imeungana na mataifa mengine ambayo yalizungumzia kwa kina haki na   uhuru wa Sahara ya Magharibi  huku ikitoa wito kwa Morocco kujiunga  tena na Umoja wa Afrika (AU) kama njia moja wapo itakayosaidia kuutafutia ufumbuzi  mgogoro huo.

Aidha Tanzania kama ilivyokuwa kwa nchi nyingine  imempongeza   na kumtia shime Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon na mshauri wake katika suala la Sahara ya Magharibi  Balozi Christopher  Ross, kuendelea na juhudi zao za  kuhakikisha kwamba mazungumao kati ya pande hizo mbili yanaendelea kufanyika kwa  njia ya uwazi, kuaminiana na kwa kuzingatia  Katiba ya Umoja wa Mataifa na maazimio mengine yahusuyo suala la  Sahara ya Magharibi.

Tanzania pia  imezitaka nchi zile ambazo zinaendelea kuyashikilia makoloni kuonyesha utashi wa kisiasa na kushirikiana na Kamati hiyo maalum ili kufikia muafaka kuhusu makoloni hayo 16 ambayo bado yanaendelea kutawaliwa.

Mbali ya Sahara Magharibi, makoloni mengine ni   Falkland Islands/Malvinas koloni linalogombewa kati ya  Uingereza na Argentina, Gibraltar ambalo pia linagombewa kati ya Uingereza na  Spain, New  Caledonia,  America Samoa, Anguilla, Bermuda, British Virgin Islands, Cayman Islands, Guam,  Montserrat, Pitcairn, Saint Helena, Turks and Caicos Islands, United States Virgin Islands, na  Tokelau. Baadhi ya makoloni hayo yanashikiliwa na Marekani.
Posted by MROKI On Friday, October 12, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo