Nafasi Ya Matangazo

October 13, 2012

Na Father Kidevu Blog, Arumeru-Arusha
Mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF) imezindua ofisi mpya katika kata ya Usariver wilayani Arumeru ikiwa ni moja kati ya kuboresha huduma za wanachama wake katika wilaya hiyo ili kuweza kuwasogezea huduma wananchi karibu zaidi.

Akizungumza katika uzinduzi huo mkurugenzi mtendaji wa NSSF , Ramadhani Dau amesema kuwa wilaya hiyo ni moja kati ya wilaya ambazo zinaiingizia michango mingi zaidi katuika mfuko huo ambapo amesema kuwa mwezi huingiza milioni 432 kwa mwezi.

Bw.Dau aliongeza kuwa mchango huo kwa mwezi ni mkubwa sana kwa kuwa ndani ya mwaka mzima ni sawa na shilingi biloni tano hali mbayo inaashiria kuwa kukiwa na ofisi hiyo karibu kutaongeza idadi ya wananchama wengine wapya katika mfuko huo.

“mfuko wa hifadhi ya jamii umeona ni vyema kama watatumia njia nzuri kuwa karibu na wananchama wake kwa kuweka ofisi hii nyinyi ili kuwapunguzia bughudha ya kufuatilia mafao pamoja na kuweka michango yenu hivyo nadhani hii itawasidia sana”alisema bw.Dau

Aidha alifafanua kuwa lengo la nssf kufungua ofisi hiyo ni ili kuwa karibu na wananchama ili waweze kuweka michango yao kwa urahisi zaidi na kuwapunguzia gharama za kufuatilia mafao wanachama ambapo ahapo awali walikuwa wanalazimika kufuata huduma zote za mfuko mjini Arusha.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa uendeshaji bw.Cricentus Magori alisema kuwa shughuli ambazo zinafanyika katika wilaya hiyo haswa mashamba makubwa ya maua ambayo yapo maeneo mbalimbali,shughuli za uchimbaji wa madini ndio chachu ya kupata michango mingi ,na wnachama wengi katika wilaya ya arumeru.

Bw.Magori alisema kuwa kwa sasa wilaya hiyo ina wanachama elfu saba ambapo alisema kuwa wameona ni muhimu kufungua ofisi ili kuwapatia huduma na kuondoa usumbufu wa kufuata huduma hizo mjini Arusha.

Katika uzinguzi huo uliofana sana ulifanyika katika kata ya usa river wilayanu arusmeru na kuwashirikisha wafanyakazi na wanachama wa mfuko huo pamoja na wadau mbalimbali
Posted by MROKI On Saturday, October 13, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo