Nafasi Ya Matangazo

October 30, 2012

Familia ya  Marehemu Emily Tilito Maro ya Uru-Kishimundu inapenda kutoa shukrani za dhati kwa ndugu jamaa na marafiki wote walioshiriki nasi katika  kufanikisha mazishi ya mdogo wetu marehemu Raymond Emily  Maro aliyefariki  dunia tarehe 2 Septemba 2012 na kuzikwa kijijini Uru Kishumundu  tarehe 6 Septemba 2012.

Mlijitolea kwa moyo wa pekee nasi tunasema tuliguswa sana na upendo na ukarimu wenu Mungu awatuze kwa wema wenu.Shukrani za pekee ziwandee madaktari  na wauguzi wa Hospitali za Seliani na St.Thomas Arusha waliofanya kazi kubwa kujitahidi kuokoa maisha ya marehemu.Pia tunatoa shukrani kwa uongozi wa TRA Makao makuu Arusha na Namanga kwa kufanikisha mazishi ya Marehemu.Tunawashukru pia Mapadri wote wa Parokia ya Kishumundu kwa kuendesha misa ya Mazishi.

Tunapenda kuwaarifu ndugu,jamaa na marafiki kuwa shughuli ya kumaliza msiba(Arobaini) itafanyika kijijini Uru-Kishumundu Jumamosi tarehe 3 Novemba 2012.Wote mnakaribishwa.
Posted by MROKI On Tuesday, October 30, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo