Nafasi Ya Matangazo

August 05, 2010

Kazi kubwa ya Polisi nchini ni Ulinzi wa raia na mali zao, Polisi Usalama barabarani (TRAFIKI) wanao wajibu mkubwa wa kuhakikisha ulinzi na usalama wa watembea kwa miguu na watumiaji wengine wa barabara unapatikana.

Watembea kwa miguu wamekuwa wakiathirika sana na wanahitaji msaada wa Trafiki hasa pale ambapo wanaona usalama wao kutoka kwa madereva wazembe ni wamashaka. Pichani ni Askari wa Usalama barabarani Unguja kisiwani Zanzibar akimvusha Mzee mkazi wa mji huo barabara ili asije kugongwa na magari au watumiaji wengine wa barabara hiyo karibu na kituo cha daladala darajani.
Trafiki wanapaswa kusimama sehemu za vivuko vya watembea kwa miguu na kuwasaidia watu wa rika mbalimbali kuvuka hasa watoto na wazee kama hawa ili kuepusha ajali zisizo za msingi tofauti na askari wengi kukalia kukamata madereva tu na kuwatoa kitu kidogo jambo ambalo linawachafua askari hao wenye dhamana ya usalama barabarani.

Posted by MROKI On Thursday, August 05, 2010 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo