Nafasi Ya Matangazo

August 04, 2010

Hizi ni zana za Kilimo ambazo zipo katika Maonesho ya Kilimo Nane nane mjini Dodoma katika banda la Wizra ya Viwanda, Biashara na Masoko.
Wananchi wakiangalia bidhaa mbalimbali zilizopo katika Banda la Wizara ya Viwanda Biashara na Masoko.
Wananchi waliotembelea banda la maonesho la Wizara ya Viwanda Biashara na Masoko wakipata maelezo katika banda hilo.
Kikosi kazi cha Wizara ya Viwanda Biashara na Masoko kilichopo katika Maonesho ya Nane nane mjini Dodoma.
Afisa wa Idara ya Bunge na Siasa Ally Abbas akitoa maelezo juu ya shughuli za Bunge na Siasa kwa Bw. Masangia alipotembela banda la Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa maonesho ya NaneNane Mkoani Dodoma.
Afisa mwandamizi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri Mkuu Aloyce H. Kway akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea banda la Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa maonesho ya NaneNane yaliyofanyika kitaifa Mkoani Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu( TAMISEMI) Mhe.Agrey Mwandri akipata maelezo kutoka kwa Maafisa waandamizi wa Idara ya Uratibu wa Maafa Bw. Edga Senga(katikati) na Bw. Gilbert Mkindi (kulia) alipotembelea banda la Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa maonesho ya NaneNane Mkoani Dodoma.

Posted by MROKI On Wednesday, August 04, 2010 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo