Nafasi Ya Matangazo

May 03, 2010

Mkurugenzi wa Taifa wa Olimpiki Maalumu, Frank Macha (kushoto) akiinua mpira wa Olimpiki utakaotumika kuzindua fainali za Kombe la Dunia 2010 zitakazoanza Juni 11 hadi Julai 11 mwaka huu Afrika Kusini, akiwa na wanaotembeza mpira huo katika nchi kadhaa duniani, Andrew Alis (wa pili kushoto) na Christian Wach. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa DHL, Dlase de Souza. Mpira huo unaotoa ujumbe maalumu wa kuhimiza walemavu kushiriki michezo ya Olimpiki, uliwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam jana ukitokea Arusha, kwa udhamini wa Shirika la Ndege la Precision Air, utakuwepo nchini kwa siku sita, na leo (Mei 4, 2010) utawekwa Uwanja wa Karume, Dar es Salaam kwa ajili ya kushuhudiwa na wananchi.Mkurugenzi wa Taifa wa Olimpiki Maalumu, Frank Macha (kushoto) akiwa ameshika mpira wa Olimpiki utakaotumika kuzindua fainali za Kombe la Dunia 2010 zitakazoanza Juni 11 hadi Julai 11 mwaka huu Afrika Kusini, baada ya kuwapokea wanaotembeza mpira huo katika nchi kadhaa duniani, Andrew Alis (wa pili kushoto) na Christian Wach.Mkurugenzi Mtendaji wa DHL, Dlase de Souza nae aliushika mpira huo.
Posted by MROKI On Monday, May 03, 2010 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo