
Watoto wakazi wa Ukonga Kipunguni Dar es Salaam Ray (kulia) na Yusra Ali wakisaidiana kupandisha ndoo ya lita kumi ya maji katika ukuta wa kisima baada ya kuchota maji hayo jana kwa matumizi yao ya nyumbani muda mfupi baada ya watoto wa darasa la kwanza kurejea nyumbani toka shule

Watoto hao wakitwishana ndoo hiyo. Amabapo Yusra aliibeba hadi nyumbani kwao.Wazazi tunapaswa kutowaruhusu watoto wa umri huu kubeba vitu vizito kwani vinaweza leta madhara katika makuzi yao hapo baadae.

Yusra akirudi nyumbani huku mguuni akiwa pekupeku.

Mwanaume nae ni mwanaume tu hapa kaka yupo nyuma hata kidumu cha lita moja yeye hana anapiga mluzi wanaenda nyumbani.

Mwenekano wa sura ya mtoto huyu inaonesha dhahiri maumivu ayapatayo kutokana na ndoo hiyo ya maji.
sio mambo hayo...ndo maana watoto wetu hawarefuki, na hawana nywele...
ReplyDelete