Akizungumza kwa njia ya simu na Kituo cha Redio cha Wapo FM, Muro amesema anayo mengi yanalolihusu Jeshi hilo na sasa wameuchokoza moto atazidi kuyapakua.
"Nasema kwa hili wameuchokoza moto...ninayo mengi ambayo nimesha yafanyia kazi juu ya Jeshi la Polisi nitaendeleza mapambano dhidi ya uovu wote" alilonga Muro.
Muro mapema jana alikamatwa na kuhojiwa kwa saa kadhaa kabla ya kuachiwa jana jioni, juu ya tuhuma za kudai na kupokea rushwa ya Shilingi Milioni 10 kutoka kwa aliyekuwa Mhasibu wa Wilaya ya Bagamoyo.






0 comments:
Post a Comment