
Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, akisalimiana na Katibu Mku wa CUF Seif Sharif Hamad,alipowasili katika uwanja wa Mkutano wa Makombeni jana Mkutano ulizungumzia zaidi umoja na utulivu Nchini,katika kusherehekea miaka46 ya Mapinduzi Zanzibar. Kulia ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni Hamad Rashid.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kaskazini Pemba Mbelwa Hamad Mbelwa akizungumza na Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Mwanamwema Shein wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa sekondari ya Makangale huko Micheweni Pemba ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 46 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Katikati ni Naibu Waziri wa mawasilino,Sayansi na teknolojia Dk Maua Daftari.

Wananchi wa Makombeni Mkoani Pemba,wakiwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Mpira Makombeni ikiwa ni shamra shamra za kuadhimisha miaka 46 ya Mapinduzi.
0 comments:
Post a Comment