Nafasi Ya Matangazo

August 01, 2015


Mtia nia ya urais kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akikabidhi fomu ya kuomba ridhaa ya chama chake kimteue kugombea nafasi hiyo kwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, Prof. Abdalaah Safari (kushoto) kwenye Makao Makuu ya chama hicho, Dar es Salaam jana. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEM. Lowassa alikuwa ni kada wa siku nyingi wa Chama cha Mapinduzi na alijiunga na Chadema hivi karibuni baada ya kuenguliwa na CCM katika mbio za kuwania kuteuliwa kuwa mgombea Urais. 
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, Prof. Abdalaah Safari (kushoto) akipeana mkono wa shukrani na Mtia nia ya urais kwa Chadema, Edward Lowassa baada ya kupokea fomu zake.
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, Prof. Abdalaah Safari akifurahia jambo na Edward Lowassa wakati akipitia fomu hizo.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na mmoja wa wanasheria mashuhuri  Mabere Marando akipitia fomu hizo
Mabere Marando akifdurahia jambo na Edward Lowassa baada ya kupokea na kuzipitia fomu zake.
Wanachama wa Chadema ambao ni wabunge wa Chama hicho wakifuatilia tukio hilo.
Mkurugenzi wa Mafunzo na Uratibu wa Kanda, Benson Kigailaakizungumza na kuelezea ukamilifu wa fomu hizo.
Lowassa akiondoka baada ya kurejesha fomu.
Posted by MROKI On Saturday, August 01, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo