Nafasi Ya Matangazo

February 20, 2014

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa PSPF, Adam Mayingu akizungumza na Waandishi wa habari pamoja na wadau wa mfuko huo katika semina ya siku moja kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo na fursa mbalimbali pamoja na mafao yanayotolewa na mfuko. 

Miongoni mwa huduma wanazotoa na ikiwa ni huduma ya fao jipya ni Mpango wa Uchangiaji kwa Hiyari  (PSS) ambapo mwanachama anatakiwa kujiunga kwa kiwango cha chini cha shilingi 10,000/= na kuchangia kadri awezavyo kila siku, wiki, Mwezi na kwa msimu kadri uwerzavyo. Semina hiyo imefanyika katika ukumbi wa JB Belmont Hotel jengo la Golden Jubilee Towers jijini Dar es Salaam.
 2Neema Muro Mkurugenzi wa Uendeshaji katika mfuko huo akitoa mada juu ya uwekezaji katika mfuko wa PSPF.
Mkurugenzi wa Fedha Masha Mushomba akizungumzia masuala ya fedha na ukusanyaji pamoja na ulipaji mafao kwa wanachama wa mfuko huo.
Andrew Nkangaa Mkurugenzi wa Tehama katika mfuko huo akizungumzia jinsi wanachama wanavyoweza kuchangia mfuko huo kwa kutumia mitandao ya simu na  kurahisisha shughuli zao za kila siku badala ya kufuata ofisi za PSPF zilipo kwa ajili ya kwasilisha michango yao.
 Wanahabari ambao ni washiriki wa semina hiyo ya siku moja wakifuatilia mada kwa umakini.
 Bloggers Shamim Mwasha wa 8020 Fashion Blog, na John Bukuku wa Fullshangwe Blog wakifuatilia mada pamoja na Sauda (kulia) kutoka EATV na Radei 5.
 Wachora katuni wao waliendelea kusikiliza huku wakichora vibonzo vyao.
Wanahabari walisikiliza kwa umakini mkubwa kila kilichoelezwa na viongozi wa PSPF.

 Meneja Mawasiliano na Masoko wa PSPF, Costantina Martin ndio alikuwa Mc wa Semina hiyo ama mchombezaji.
 Mwanahabari kutoka ITV, Fatma Nyangasa akipitia kipeperushi kilicho na maelezo juu ya namna ya kujiunga na Mpango wa Uchangiaji wa Hiari (PSS) ambapo gharama ya chini ni 10,000 tu kujiunga na unaweza ukawa unatuma michango yako kila siku, wiki, mwezi au kwa msimu maalum kadri uwezavyo.
 Hizi ni huduma mbalimbali zitolewazo na PSPF
 Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji, Gabriel Silayo nae aleelezea mikakati ya PSPF.
 Washiriki wa semina walimsikiliza Silayo vyema.
Mwanahabari mkongwe, Deogratius Mushi akisema neno la shujkrani kutokana na kile alichokipata wa niaba ya washiriki wote.
Posted by MROKI On Thursday, February 20, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo