Nafasi Ya Matangazo

July 26, 2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe limeungana na wananchi wa Mji Mdogo wa Mlowo, Wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Songwe kufanya zoezi la usafi katika eneo la Stendi Mpya ya Mabasi ya Mlowo ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha usafi wa mazingira, kuimarisha afya ya jamii na kuendelea kujenga ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na wananchi.

Zoezi hilo la usafi lililofanyika Julai 26, 2026 katika Stendi Mpya ya Mabasi ya Mlowo Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe na kuongozwa na Mkuu wa Polisi Mkoa wa Songwe, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Maria Kway, alisema kuwa ushirikiano waliouonesha katika kuhakikisha mazingira yanakuwa safi na salama kwa wafanyabiashara, wasafiri na wananchi wote wanaotumia eneo hilo uendelee na uwe utamaduni wa maisha ya kila siku.

Aidha, ACP Kway aliwahimiza wananchi hao kuzingatia usafi katika maeneo wanayofanyia biashara kwa kuhakikisha wanakuwa na vifaa vya kuhifadhia taka na kuweka utaratibu wa kufanya usafi kwa pamoja kila wiki ili kudumisha mazingira safi na yenye afya.

Mwisho, ACP Kway aliwakumbusha wananchi hao kuendelea kutii sheria za nchi bila kushurutishwa kwa kujiepusha na vitendo vya uhalifu, badala yake waelekeze nguvu zao katika kufanya kazi halali na kujipatia kipato cha halali, huku akiwasisitiza kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe katika kuzuia na kutokomeza uhalifu ili kudumisha amani na usalama wa Mkoa wa Songwe.






Posted by MROKI On Sunday, July 26, 2026 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo