Nafasi Ya Matangazo

June 04, 2026



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University) kutoka kwa Mkuu wa Chuo hicho Profesa Oleg Yastrebov kwenye hafla iliyofanyika Chuoni hapo Moscow nchini Urusi, tarehe 04 Juni, 2026. Rais Mhe. Dkt. Samia ametunukiwa Shahada hiyo ya Uzamivu kutokana na mchango wake katika Mageuzi ya sekta ya Elimu, juhudi zake za kuimarisha Diplomasia ya Tanzania, pamoja na mchango wake katika kuimarisha hadhi ya Tanzania Kimataifa ikiwemo kupitia sekta ya Utalii.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi wa Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University), Wanafunzi wa Chuo hicho, wageni mbalimbali baada ya kutunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) kwenye hafla iliyofanyika chuoni hapo Moscow nchini Urusi, tarehe 04 Juni, 2026. 










Viongozi wa Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University), Wanafunzi wa Chuo hicho pamoja na wageni mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya Kutunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Chuoni hapo Moscow nchini Urusi tarehe 04 Juni, 2026. 


Posted by MROKI On Thursday, June 04, 2026 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo