Benki
ya NMB imetangaza udhamini wa Sh milioni 150 kufanikisha msimu wa nane wa
Mashindano ya Kombe la Mkuu wa Majeshi—CDF Cup 2026—yatakayofanyika Dar es
Salaam kuanzia Julai 6 hadi 17.
Mashindano
hayo yatahusisha michezo 13 na timu kutoka Kamandi ya Makao Makuu ya JWTZ,
Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu, Kamandi ya Jeshi la Anga, Kamandi ya Jeshi la
Wanamaji, Kamandi ya Jeshi la Akiba na Kamandi ya Jeshi la Kujenga Taifa.
Mkuu
wa Idara ya Wateja Binafsi wa Benki ya NMB, Aikansia Muro, alisema udhamini huo
unaendeleza ushirikiano wa benki hiyo na majeshi katika kukuza michezo,
kuimarisha ushindani na kujenga umoja, afya thabiti na mshikamano miongoni mwa
washiriki.
Mashindano
yatafunguliwa Julai 6 katika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, huku yakitarajiwa
kutoa jukwaa la kukuza vipaji, kuimarisha utimamu wa mwili na afya ya akili
pamoja na kujenga mahusiano mema kwa washiriki.
Mkuu
wa Idara ya Wateja Binafsi wa Benki ya NMB, Aikansia Muro (kushoto), akikabidhi
hundi mfano ya udhamini wa Sh milioni 150 kwa Mwenyekiti wa Kamati ya
Maandalizi ya CDF Cup 2026, Brigedia Jenerali Saidi Hamis Saidi (katikati),
jijini Dar es Salaam.
Mashindano
hayo yatafanyika kuanzia Julai 6 hadi 17, yakishirikisha timu za kijeshi katika
michezo 13.



















0 comments:
Post a Comment