Nafasi Ya Matangazo

June 17, 2025



Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete ameshiriki na kuhutubia Kongamano la PPRA lililolenga kujadili Ununuzi wa umma na Ukuzaji wa kampuni za wazawa na makundi maalum kwa ukuaji wa Uchumi Jumuishi katika zama hizi za mabadiliko ya teknolojia/ Kidigitali
 
Kongamano hilo limefanyika Juni 16, 2025 Jijini Arusha ambapo katika hotuba yake Kikwete amesisitiza umuhimu wa kuendelea kutambua mabadiliko mbalimbali yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dr. Samia Suluhu Hassan , Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo pamoja na mambo mengine yanalengwa kuwasaidia na kukuza ustawi wa Watu wenye mahitaji maalum.
 
Kikwete alibainisha kwa kuwakumbusha mambo 6 yaliyofanywa na  Serikali ya awamu ya sita katika kuwawezesha vijana na watu wenye ulemavu ili waweze kujiinua kiuchumi ikiwemo maelekezo ya kisheria ya kuendelea kutenga asilimia 30 ya zabuni za ununuzi wa umma.
 
Aidha, aliwakumbusha umuhimu wa kutoa elimu na kuwashirikisha wadau muhimu katika jamii wakiwemo Madiwani na Wakurugenzi wa Halmashauri, Manispaa na Majiji ili elimu ya kuwepo kwa fedha maalum zinazotengwa toka kwenye manunuzi ya Umma ijulikane.
 
“Moja ya changamoto kubwa kwa sasa ni ufahamu hafifu wa kuwepo kwa fedha hizi. Umuhimu na msisitizo kama huu umesaidia sana vijana, wanawake na wenye ulemavu kukimbilia zile asilimia 10 zinazotengwa na Halmashauri kutoka kwenye mapato ya ndani,”alisema Kikwete.
Posted by MROKI On Tuesday, June 17, 2025 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo