Nafasi Ya Matangazo

October 28, 2024

Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Peter Kisenge watatoa 
huduma za tiba mkoba zijulikanazo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services kwa kufanya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam  na mikoa ya jirani.
 
Huduma hii itatolewa bila malipo kwa watoto na watu wazima wakiwemo Waandishi wa Habari lengo likiwa ni kusogeza huduma za kibingwa za matibabu ya moyo karibu zaidi na wananchi.

Matibabu haya yatatolewa tarehe 29-30/10/2024 kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni katika Kliniki ya JKCI Kawe iliyopo Kawe jengo la Mkapa Health Plaza barabara ya Tuari.

Kutakuwa na wataalamu wa lishe watakaotoa elimu ya lishe bora itayayowapa wananchi uelewa wa kufuata mtindo bora wa maisha na kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo ya moyo yanayoweza kuepukika kwa kufuata ushauri wa kitaalamu.
 
Tunawaomba wananchi mjitokeze kwa wingi kupima afya zenu kujua kama mna matatizo ya moyo ili kuanza matibabu mapema kwa atakayegundulika kuwa mgonjwa.

Kwa taarifa zaidi wasiliana kwa simu namba 0783922571 na 0680280007 Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kliniki ya Kawe.
Posted by MROKI On Monday, October 28, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo