Nafasi Ya Matangazo

August 29, 2024


Naibu waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali inaendelea na majadiliano na Kampuni za Nishati za Kimataifa (International Energy Companies - IEC’s) kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa Kuchakata na Kusindika Gesi asilia kuwa Kimiminika – LNG na yakikamilika Serikali itaupeleka kwenye hatua inayofuata.

Mhe. Kapinga amesema hayo leo Agosti 29, 2024 bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Mhe. Joseph Khenani aliyetaka  kufahamu lini Serikali  itapeleka bungeni mkataba kati ya Tanzania na Wawekezaji wa Gesi asilia wenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni 70 kwa ajili ya kujadiliwa.
Posted by MROKI On Thursday, August 29, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo