Nafasi Ya Matangazo

April 03, 2024

Sylvester Joseph Kainda.
 Jaji Mteule wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi kama ifuatavyo: 

Amemteua Bw. Sylvester Joseph Kainda kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Kabla ya uteuzi huu Bw. Kainda alikuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani.

Amemteua Bi. Eva Kiaki Nkya kuwa Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania. Kabla ya uteuzi huu Bi. Nkya alikuwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Amemteua Bw. Chiganga Mashauri Tengwa kuwa Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Kabla ya uteuzi huu Bw. Tengwa alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Geita.    
Posted by MROKI On Wednesday, April 03, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo