Nafasi Ya Matangazo

July 03, 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 02 Julai, 2023 amefanya mabadiliko madogo ya Wakuu wa Wilaya kama ifuatavyo:

Ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mwanahamisi Athumani Munkunda na kumteua Mobhare Holmes Matinyi (pichani) kuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke.

Ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Abel Yeji Busalama. Amemhamisha  kituo Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mjini, Hashim Shaib Mgandilwa kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi.
Amemteua James Wilbert Kaji kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mjini.

Posted by MROKI On Monday, July 03, 2023 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo