Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mwanasiasa ambaye pia ni mmoja wa Viongozi Wakuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Antiphas Lissu leo tarehe 16 Februari, 2022 katika Jiji la Brussels nchini Ubelgiji.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mwanasiasa ambaye pia ni mmoja wa Viongozi Wakuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Antiphas Lissu leo tarehe 16 Februari, 2022 katika Jiji la Brussels nchini Ubelgiji.
*********
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amekutana leo na
kufanya mazungumzo mafupi na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA), Mhe. Tundu Lissu.
Taarifa iliyotolewa na kusainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Zuhura
Yunus imesema Mazungumzo hayo yamefanyika baada ya Rais Samia
kukubali maombi ya kiongozi huyo wa Chadema kukutana naye na kuzungumza jijini
Brussels.
Aidha katika mazungumzo hayo Mhe. Rais na Makamu
Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, walizungumza masuala mbalimbali yenye
maslahi na ustawi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Mwanasiasa ambaye pia ni mmoja wa Viongozi Wakuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Antiphas Lissu leo tarehe 16 Februari, 2022 katika Jiji la Brussels nchini Ubelgiji.
0 comments:
Post a Comment