Nafasi Ya Matangazo

September 30, 2019

Mbunge wa Jimbo la Vwawa ambaye pia ni Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga akimkabidhi vifaa vya michezo nahodha wa timu ya Hasamba Fc Ndg Waziri Nzunda wakati wa kilele cha Mashindano ya "HASUNGA CUP 2019" yaliyofanyika katika katika viwanja wa Chama Cha Mapinduzi Mkoani Songwe leo tarehe 29 Septemba 2019. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Mbunge wa Jimbo la Vwawa ambaye pia ni Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga akisalimiana na waamuzi kadhalika wachezaji wakati wa kilele cha Mashindano ya "HASUNGA CUP 2019" yaliyofanyika katika katika viwanja wa Chama Cha Mapinduzi Mkoani Songwe leo tarehe 29 Septemba 2019.
Mbunge wa Jimbo la Vwawa ambaye pia ni Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga akisalimiana na mashabiki wa mpira wakati wa kilele cha Mashindano ya "HASUNGA CUP 2019" yaliyofanyika katika katika viwanja wa Chama Cha Mapinduzi Mkoani Songwe leo tarehe 29 Septemba 2019.
Moja ya mshambuliaji wa timu ya Hasamba Fc akiwatoka wachezaji wa timu ya Ihanda Fc wakati wa kilele cha Mashindano ya "HASUNGA CUP 2019" yaliyofanyika katika katika viwanja wa Chama Cha Mapinduzi Mkoani Songwe leo tarehe 29 Septemba 2019.
Mbunge wa Jimbo la Vwawa ambaye pia ni Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga akizungumza na wachezaji kabla ya mchezo wa fainali wakati wa kilele cha Mashindano ya "HASUNGA CUP 2019" yaliyofanyika katika katika viwanja wa Chama Cha Mapinduzi Mkoani Songwe leo tarehe 29 Septemba 2019.
***************
Na Mathias Canal, Songwe
Mashindano ya "HASUNGA CUP 2019" Leo tarehe 29 Septemba 2019 yamefika ukomo Wilayani Mbozi Mkoani Songwe ambapo timu ya Hasamba Fc ndiyo iliyoibuka kidedea na kunyakua zawadi kwa kuibamiza bila huruma timu ya Ihanda Fc kwa jumla ya Penati 7 kwa 6

Timu hiyo ya Hasamba Fc imeambulia ushindi huo wa goli 7 kwa 6 mara baada ya dakika 90 za mchezo kumalizika kwa timu hizo kutoka suluhu magoli yaliyofungwa na mshambuliaji Asili Mnkondya wa timu ya Ihanda mnamo dakika ya 20 huku Beny Mgonde akiisawazishia timu yake mnamo dakika ya 72 ya mchezo huo.

Michuano hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Mbunge wa Vwawa na kuendeshwa kwa umahiri mkubwa, ilizinduliwa mwezi Machi 2019 katika uwanja wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Songwe huku ikizikutanisha timu 18 zilizotokana na muunganiko wa timu za vijiji katika kata hizo 18 katika Jimbo la vwawa.

Akizungumza katika kilele cha Mashindano hayo kilichofikia ukomo katika katika viwanja wa Chama Cha Mapinduzi Mkoani Songwe, Mbunge wa Jimbo la Vwawa ambaye pia ni Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga amesema kuwa mashindano hayo yalianzishwa kwa lengo mahususi kwa ajili ya kubaini vipaji vya vijana kwa ajili ya kuunda timu itakayoshiriki ligi daraja la nne na hatimaye ligi kuu Tanzania bara.

Amesema kuwa mashindano hayo pia yamekuwa ni sehemu ya kuhamasisha wananchi pamoja na wadau mbalimbali ambayo yamewaimarisha vijana hususani katika kuonyesha vipaji vyao.

Katika mashindano hayo Mshindi wa kwanza ambayo ni timu ya Hasamba Fc amekabidhiwa zawadi ya Seti moja ya jezi, Seti moja ya soksi na kitita cha Shilingi laki tatu.

Mshindi wa pili timu ya Ihanda Fc imepewa zawadi seti moja ya jezi, seti moja ya soksi na kitita cha shilingi 200,000, Mshindi wa tatu yeye amekabidhiwa seti moja ya jezi na kitita cha Shilingi 100,000 huku mshindi wan ne akijinyakulia seti moja ya jezi pekee.

Katika hotuba yake Mbunge huyo wa Jimbo la Vwawa na Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga aliwapongeza viongozi wote na timu zote zilizoshiriki ligi hiyo kwani bila wao kusingekuwa na mafanikio yenye tija.

Mhe Hasunga aliwahakikishia wananchi kuwa mashindano hayo yatakuwa endelevu ili kutekeleza mpango mkakati wa uimarishaji na uboreshaji wa michezo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020 ibara ya 161.
Posted by MROKI On Monday, September 30, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo