Nafasi Ya Matangazo

February 09, 2019

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akiongoza kikao kazi ngazi ya Mawaziri kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). Pamoja na mambo mengine kikao hicho kimejadili masuala ya Muungano ikiwa ni kikao cha utangulizi kabla ya kikao cha Kamati ya Pamoja kitakachoongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. Kikao hicho kimehudhiriwa pia na Manaibu Waziri na Makatibu Wakuu wa Tanzania Bara na Zanzibar
 Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akichangia katika kikao kazi cha Mawaziri wa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar kujadili masuala ya Muungano. Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu Bunge Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama. Kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Uwekezaji Mhe. Angela Kairuki.

Sehemu ya Wajumbe wa kikao hicho ambao ni Mawaziri, Manaibu Waziri na Makatibu Wakuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) wakifuatilia kikao hicho, kilichofanyika katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma.
Posted by MROKI On Saturday, February 09, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo